Kilimanjaro Stars yapangwa mchekea Chalenji Cup 2013





BARAZA la Shirikisho la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) linatarajia kutangaza ratiba rasmi ya michuano ya Kombe la Chalenji itakayofanyika nchini Kenya. tayari makundi ya michuano hiyo yametangazwa.
Tanzania Bara inayowakilishwa na Kilimanjaro Stars yenyewe imepangiwa kundi mchekea la B pamoja na timu za Zambia ambao ni waalikwa, Burundi na Somalia.
Wawakilishi wengine wa Tanzania, Zanzibar Heroes ya Zanzibar yenyewe imepangwa kundi A na wenyeji Kenya, Ethiopia na Sudan Kusini, wakati kundi la kifo ni kile la C lenye timu za Uganda ambao ni mabingwa watetezi , Rwanda, Sudan na Eritrea.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi lake kuanzia Novemba 27 jijini Nairobi kuwania taji hilo ambalo kwa miaka mingi limetawaliwa na Waganda.
MAKUNDI YALIVYO CHALENJI 2013:
KUNDI A- Kenya, Ethiopia, Zanzibar, South Sudan

KUNDI B- Tanzania, Zambia, Burundi and Somalia

KUNDI C- Uganda, Rwanda, Sudan and Eritrea.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List