WASANII KIBAO WAJITOKEZA KUSHIRIKI MKESHA WA MBIO ZA UHURU MARATHON



Katibu wa kamati ya maandalizi ya mbio za uhurumarathon, Innocent Melleck, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam juu ya maandalizi na wasanii watakaoshiriki kwenye mkesha wa Uhuru utakaofanyika viwanja vya Leaders Club baada ya kukamilika kwa mbio za uhuru. Kushoto ni katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania Selemani Nyambui.
*********************************
Na Mwandishi Wetu, Dar
ZIKIWA zimebaki siku chache kwa ajili ya shindano la mbio ndefu za Uhuru, 'Uhuru Marathon', kufanyika, wasanii watakaotoa burudani siku ya mkesha wa uhuru wapania kufanya kweli.
Wasanii wanaotarajiwa kutoa burudani ni Roma Mkatoliki, Joh Makini, G Nako, Nick wa Pili, Mrisho Mpoto, Mrisho Mpoto, TMK Wanaume, Mfalme Siboka na kundi la Twanga Pepeta.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wasanii hao walisema wanashukuru kupewa heshima kubwa kutumbuiza siku hiyo na hasa ukichukulia umuhimu wa amani, umoja na mshikamano miongoni mwetu.
“Nitafanya makamuzi ya kweli siku hiyo na watu wategemee mistari iliyokwenda shule,” alisema Roma Mkatoliki, huku Mrisho Mpoto akidai ana vitu vikali zaidi atakavyoweka hadharani siku hiyo.
Naye Katibu wa Kamati ya Uhuru Marathon, Innocent Melleck alisema, homa ya mbio hizo imepanda, hasa baada ya kujitokeza kwa wanariadha wengi wa mataifa, kutoka nchi mbalimbali.
Melleck alisema, mbali na wengi kujitokeza bado anaamini wengi wataendelea kujiandikisha ili kufanikisha lengo la mbio hizo.
Aidha alisema kuwa usajili bado unaendelea kwa wale wanaotaka kushiriki ambapo fomu zitakazotolewa kwa mshiriki wa kilomita 3 atalipa Sh 100,000 yule wa kilomita 5 Sh 2,000 na washiriki wa kilomita 21 na 42 watalipia Sh 6,000.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List