Mahakama moja nchini Libya
imemuhukumu kumyonga mwana wa aliyekuwa rais wa taifa hilo Gaddafi,Saif
al Islam na wengine wanane kufuatia uhalifu wa kivita uliohusishwa na
mapinduzi ya mwaka 2011.
Walikuwa wameshtakiwa pamoja na washirika
wengine wa kiongozi huyo aliyeondolewa mamlakani kwa kujaribu kazima
maandamano wakati wa mapinduzi hayo.Saif al Islam hakuwepo mahakamani na alitoa ushahidi wake kupitia teknolojia ya kanda ya video.
Kwa sasa Saif anazuiliwa na kundi moja la waasi la zamani katika mji wa Zintan ambao wamekataa kumuachilia huru.
0 comments:
Chapisha Maoni