TTCL, TSN, TCRA, AICC, YARA WASHIRIKI KIKAMILIFU MAONESHO YA WAKULIMA NANE NANE DODOMA 2013


Kampuni Kongwe ya Mawasiliano ya Simu Tanzania (TTCL) nayo ipo katika Viwanja vya Nzuguni, kuelimisha umma juu ya huduma zake. Pichani ni Maofisa wa Kampuni hiyo Thomas Lemunge ambaye ni Afisa Biashara wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (katikati) akitoa elkimu kwa mwananchi huku Afisa Habari, Amanda Luhanga akifuatilia.
 Baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wakiwa katika picha ya pamoja katika banda lao lililopo ndani ya Viwanja vya Nzuguni Mjini Dodoma yanapofanyika Maonesho ya Kitaifa ya Wakulima Nane Nane. Mwaka huu TCRA wanakuambia 'FUTA-DELETE' ujumbe wowote usio na maana katika simu yako au mtandao wa Barua pepe. Ila Father Kidevu Blog, inaongezea Ujumbe 'PUUZIA-IGNORE' taarifa yeyote isiyo na manufaa kwa jamii katika Mitandao ya Kijamii.
 Naibu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mwasiliano Tanzania (TCRA) anaeshughulika na Uratibu wa Kanda, Victor Nkya akitoa elimu ya FUTA-DELETE kwa vijana waliotembelea banda hilo leo.

 Kikosi kazi cha Kampuni ya Magazeti ya Serikali Tanzania Standard Newspapers (TSN) Limited ambacho kipo ndani ya viwanja vya Nzuguni katika Banda la Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo katika Maonesho ya siku ya Wakulima Nane Nane yaliyoanza Agosti Mosi na kutaraji kumalizika Agosti 8, 2013 kitaifa Mkoani Dodoma. Kushoto ni Afisa Masoko, Francis Kihinga akiwa na Afisa Mauzo na Masoko, Chikira Mgheni. TSN ndio wachapishaji na wasambazaji wa Magazeti ya Daily News, Sunday News, HABARILEO, HABARILEO Jumapili na SpotiLEO.
 Afisa Masoko wa TSN, Francis Kahinga akigawa majarida ya Elimika na Academy kwa wanafunzi walio tembelea banda la TSN. TSN ndio wachapishaji na wasambazaji wa Magazeti ya Daily News, Sunday News, HABARILEO, HABARILEO Jumapili na SpotiLEO.
 Kampuni Kongwe ya Mawasiliano ya Simu Tanzania (TTCL) nayo ipo katika Viwanja vya Nzuguni, kuelimisha umma juu ya huduma zake. Pichani ni Maofisa wa Kampuni hiyo Thomas Lemunge ambaye ni Afisa Biashara wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (katikati) akitoa elkimu kwa mwananchi huku Afisa Habari, Amanda Luhanga akifuatilia.
 Wafanyakazi mbalimbali wa TTCL wakiwa bandani hapo wakitoa elimu ya huduma zao.
Ofisa Masoko na Utafiti wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), Linda Nyanda, akiwapa maelezio wanafunzi wa kidato cha tatu wa Sekondari ya Maria de-Mathias ya mjini Dodoma juu ya shughuli mbalimbali za AICC walipotembelea banda hilo katika Maonesho ya Wakulima nane nane katika Uwanja wa Nzuguni mjini Dodoma.
Ofisa Habari Mwandamizi na Itifaki wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), Catherine Kilinda akiwapa maelezio wanafunzi wa kidato cha tatu wa Sekondari ya Maria de-Mathias ya mjini Dodoma juu ya shughuli mbalimbali za AICC walipotembelea banda hilo katika Maonesho ya Wakulima nane nane katika Uwanja wa Nzuguni mjini Dodoma.
Afisa Mauzo wa Kampuni ya YARA Tanzania Limited, Catherine Assenga (kushoto) akimsadia mwananchi aliyetembelea banda lao lililopo ndani ya Banda la NMB katika Viwanja vya Maonesho Nane Nane, Nzuguni Mjini Dodoma. YARA ndio wasambazaji wa Mbolea CHAPA MELI.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List