Mahakama ya kimataifa ya Uhalifu wa kivita,ICC imesema kuwa imepata ushahidi wa kutosha kumfungulia mashitaka mbabe wa kivita wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo Bosco Ntaganda.
Ntaganda anashutumiwa kwa makosa ya Ubakaji, mauaji na hata kuwasajili watoto wadogo kama wapiganaji wakati wa vita vya mashariki mwa DRC.