KING CLASS MAWE ASAINI MKATABA WA KUPAMBANA NA CHEKA FEB 8 PTA SABASABA




BONDIA bora wa mwaka 2013,2014 katika uzito wa  KG 63  Ibrahimu Class 'King Class Mawe' ame saini mkataba wa kupambana na Cosmas Cheka Feb 8 mwaka huu katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam
Mara baada ya kusaini mkataba huo wa kucheza raundi 10 za ubingwa wa Taifa kg,60 amesema atafanya mazoezi ya kutosha kuhakikisha ana msambalatisha mpinzani wake raundi za awali kwa kuwa alikuwa anachonga sana juu yake

mpambano huo uliodhaminiwa na Promota Maarufu nchini Jay Msangi utakuwa na msisimko wa aina yake kutokana na mabondia hawo kuwa gumzo katika ulimwengu wa masumbwi ndani na nje ya nchi ya tanzania

King Class aliongeza kwa kusema kuwa nipo fiti nimejiandaa na ninasubili tu kuvishwa ubingwa huo wa taifa kwani Cheka ana ujanja kwangu mbinu zake zote nimesha zikamata

King Class Mawe anae nolewa na jopo la makocha wanao ongozwa na Habibu Kinyogoli 'Masta' Rajabu Mhamila 'Super D' Kondo Nasoro 

Bondio huyo amewashukulu wadau wa mchezo wa ngumi kwa kumuwezesha kuchaguliwa kuwa bondia bora wa mwaka katika uzito wake kwa kuwapita mabondia wengine wanne na yeye kuibuka kidedea katika kin'yan'gan'yiro hicho
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List