Makamu wa rais mteule wa Marekani Mike Pence, amethibitisha kuwa Mitt Rombey anaweza kupewa wadhifa wa Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni.
Taarifa hiyo iliyotangazwa na kituo cha Fox News, inajiri baada ya rais Mteule Donald Trump kukutana na bwana Romney, mwanachama wa Republican ambaye alimkosoa wakati wa kampeni.
Kuna uvumi kuwa wadhifa huo ulizungumziwa wakati wa mkutano kati ya viongozi hao.
Hakuna hata mmoja kati yao alitoa taarifa za mkutano wao uliofanyika siku ya Jumamosi.
Mwezi machi wati wa mchujo, bwana Romney alisema kuwa Trump hana tajriba ya kuwa rais naye Trump akajibu kuwa Romney ni mgombea aliyeshindwa.
MKURUGENZI WA MAWASILIANO YA RAIS IKULU BAKARI MACHUMU AKUTANA NA WANABLOGU
NA WAZALISHAJI MAUDHUI MTANDAONI IKULU DAR
-
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bw. Bakari Machumu akiwa na
viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na Waandishi wa Habari wa
Mtandaoni, pa...
Saa 14 zilizopita
0 comments:
Chapisha Maoni