Video ya ‘Dume Suruali’ ya Mwana FA akiwa na Vanessa Mdee pamoja na video ya ‘Muziki’ ya Darassa akiwa na Ben Pol ndizo video za muziki wa rap Tanzania zinazoongoza kwa kuangaliwa zaidi kwenye mtandao wa YouTube kwa muda mfupi hivi sasa.
Video hizo zimeonekana kutoana nduki kwa mashabiki wao kuziangalia mara nyingi zaidi zikigusa rekodi ya kuangaliwa zaidi ya mara milioni moja ndani ya kipindi kisichozidi wiki mbili tangu zilipopandishwa mtandaoni.
Muziki ya Darassa imeshaangaliwa zaidi ya mara milioni 1.43 tangu ilipopandishwa kwenye mtandao huo Novemba 23 mwaka huu huku ‘Dume Suruali’ ikiangaliwa zaidi ya mara milioni 1.13 tangu ilipowekwa YouTube Novemba 25 mwaka huu.
Hii inaonesha kuwa hivi sasa wasanii wanaungwa mkono zaidi na mashabiki wao kwa kuangalia video zao kwenye mtandao kutokana na uwepo wa mapinduzi ya kiteknlojia, ambapo mamilioni ya Watanzania sasa wanaweza kupata ‘internet’ kwenye simu zao.
NGORONGORO LADIES MGUU SAWA MASHINDANO YA SHIMMUTA MOROGORO
-
Timu ya mpira wa Netiboli na mpira wa wavu ya Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro imewasili mkoani Morogoro tarehe 25 Novemba 2025, imeendelea na
program ya...
Saa 18 zilizopita
0 comments:
Chapisha Maoni