KITUO cha afya cha Chalinze kilichopo Kitongoji cha Bwilingu halmashauri ya Chalinze Bagamoyo Mkoa wa Pwani kimeanza kuwafanyia operesheni wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo kituoni hapo.
Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mwanasheria Ridhiwani Kikwete ndiye aliyechokonoa hoja hiyo alipomtaka Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo kumpatia uhakika wa jambo hilo ambalo analisikia kwa watu kwamba Kituo hcho kimeshaanza zoezi la kuwafanyia upasuaji wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo.
"Nimesikia maneno kutoka kwa wakazi wakisema kwamba Kituo chetu cha afya Chalinze kimeshaanza kuwafanyia upasuaji wagonjwa wanaokwenda kwa ajili ya huduma hiyo, Mganga Mkuu tunaomba ulitaarifu Baraza hili taarifa hizo zilizo njema zina ukweli gani?," aliuliza Ridhiwani.
Akijibu swali hilo, Dr. Isaack Makungu aliwathibitishia Madiwani hao kwamba taarifa hizo zina ukweli na tayari akina mama 10 wajawazito wameshapatiwa huduma ya upasuaji kisha kupata watoto wakiwa salama na afya njema pamoja na wazazi wenyewe wakiwa na afya iliyo njema.
"Ni kweli Kituo chetu kimeshaanza kazi ya kuwafanyia upasuaji akina mama wajawazito ambao wamebainika hawana uwezo wa kusukuma mtoto ambapo watu kumi tumeshawapatia huduma hiyo wakiwa salama wao pamlja na watoto wao," alisema Dr. Makungu.
Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Said Zikatimu aliliambia Baraza hilo kwamba hatua hiyo ni faraja kwao kwani itasaidia mambo mengi kwanza kuwapunguzia saafari ndefu ya kwenda Tumbi, Bagamoyo au Muhimbili, poa mafuta ambayo yalikuwa yanatumika kusafirisha wagonjwa kweda maeneo nayo.
"Taarifa hiyo ni faraja kwetu kwani itasaidia wagonjwa ambao awali walikuwa wanasafirishwa kwenda Tumbi, Bagamoyo au Muhimbili, lakini tunatakiwa kujenga uzio kutoka chumba cha upasuaji kwenda wodini ili mgonjwa anapotoka kufanyiwa upauaji asiwe anaonekana na watu wengine," alisema Zikatimu
- Blogger Comment
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Inaendeshwa na Blogger.
About Me
Wanaofuata
TANGAZO
My Blog List
-
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masum...Miaka 5 iliyopita
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye kwa sasa anamnowa bondia Sunday Kiwale 'Moro Best' kwa aj...Miaka 5 iliyopita
-
BONDIA MAKUBI ATAMBA KUMPIGA ABDALLAH MA MOROGORO OKTOBA 4 KATIKA UKUMBI WA 361 MWENGE - Na Mwandishi wetu Bondia Ibrahim Makubi yupo kambini kwa ajili ya mazoezi yake ya kumkabili bondia abdallah kingolwira wa ( morogoro ) katika pambano l...Miaka 5 iliyopita
-
JUMA CHOKI AJIANDAA NA MASHINDANO YA KING OF THE RING JULAI 28 - Bondia Ibrahimu Makubi kushoto akioneshana umwamba na Juma Choki wakati wa Mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Super D iliyopo shule ya Uhuru Kariakoo...Miaka 5 iliyopita
-
0 comments:
Chapisha Maoni