CRDB YATUMIA MILIONI 50 KUKARABATI WARD YA WAJAWAZITO HOSPITALI YA BUGANDO MWANZA



Mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo akikata utepe kuashiria ufunguzi ward ya wajawazito katika hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza ambapo CRDB iliifunga kwa muda ward hiyo ilikuifanyia ukarabati madhubuti na kuwa ya kisasa zaidi. Kutoka kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza, Mkurugenzi wa BMC Prof. Charles Majinge, Mkurugenzi mtendaji wa CRDB Dr. Charles Kimei (aliyenyanyua mkono), Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga na mmoja kati ya maafisa wa CRDB. 
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo akifungua pazia la bango la wadhamini katika hafla ya kukabidhi ward ya wajawazito Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza iliyokarabatiwa na CRDB Benki. 
Pia CRDB imekabidhi mablanketi, vyandarua, vitanda na mashuka pamoja na mapazia ya kusitiri huduma maalum kwa ward ya wajawazito Bugando.
Huduma ya Afya ya mama na mtoto inakabiliwa na changamoto nyingi sana moja wapo ni ugonjwa wa malaria ambao umekuwa moja ya vyanzo vikuu vya vifo vya watoto nchini, kwa kuliona hilo CRDB wamehakikisha kila kitanda kina neti yenye ukubwa wa kutosha.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List