WANANCHI WA MOROGORO BWILA CHINI NA JUU WAGOMEA KUPISHA MRADI WA BWAWA LA KIDUNDA KWA KUWA DAWASA WAMETOA MALIPO KIDUCHU.WAKATI BENK YA DUNIA IMETOA FEDHA NYINGI ZA FIDIA KWA WAKAZI HAO.

Wanakijiji wa Bwila juu,Bwila chini na Kibulumo  kata ya Selembala tarafa ya Mvuha,Mkoani Morogoro wamesema kuwa awataupisha mradi wa Bwawa kubwa la mji la  Kidunda hadi hapo Serikali itakapotatua suala la kulipwa Fidia stahiki kwa wakazi wa eneo hilo.

Wananchi hao wamedai kuwa baadhi ya wakazi wa maeneo hayo wamekuwa wakiishi katika mazingira magumu hasa wakazi wa vijiji hivyo  vilivyoguswa na mradi wa Bwawa la maji Kidunda.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Kibulumo Juma Majile amesema wakati wamefika kuelezea mradi wa maji jinsi utakavyokuwa wananchi walikuwa na matumaini makubwa lakini tofauti na hivyo mradi umekuwa kama chanzo cha kutaka kuwaingiza katika janga la Umaskini.

Mkurugenzi Halmashauri ya Morogoro Vijijini Nd,Yona Maki amekiri kupokea malalamiko ya fidia kutoka kwa Wananchi walioguswa na Mradi huo wa Bwawa Kubwa la Maji Kidunda.

Serikali imejipanga kujenga Mradi wa Bwawa kubwa la maji lenye ujazo wa mita milioni 190 litakalo kuwa likitoa huduma katika mikoa ya Dar es salaam,Pwani na Morogoro kwa kusaidiwa na Benki ya Dunia.

Ofisi ya DAWASA
Afisa Habari Msaidizi wa DAWASA aliyejibu majibu ambayo si ya kiungwana kwa Waandishi wa habri


Mkurugenzi Halmashauri ya Morogoro Vijijini Nd,Yona Maki

Ofisi ya mkuu wa wilaya Morogoro.

Ofisi ya mkuu wa wilaya Morogoro.

Wanakijiji wakitawanyika baada ya mkutano kushindwa kutoa majibu ya kufikia muafaka.

Wanakijiji wakitawanyika baada ya mkutano kushindwa kutoa majibu ya kufikia muafaka.

Baadhi ya nyumba za wanakijiji waliopo katika eneo la Mradi

Baadhi ya nyumba za wanakijiji waliopo katika eneo la Mradi

Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Kibulumo Juma Majile

Baadhi ya nyumba za wanakijiji waliopo katika eneo la Mradi

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List