KAMPUNI YA IJUMBA ENTERPRISES YAJA NA SULUHISHO LA AJALI ZA BODABODA



pikipikiKampuni ya Ijumba Enterprises inatarajia kuzindua mradi wa Safari Salama {Safer Journey} katikati ya mwezi November, 2013.
Mradi huu unalenga waendesha pikipiki za miguu miwili na mitatu yaani bodaboda. Mradi unalenga kuwaongezea waendesha bodaboda elimu ya udereva salama na kuzijua sharia za usafirishaji.
Kampuni hiyo imegundua kwamba ajali nyingi zinazotokana na bodaboda kwa kiasi kikubwa husababishwa na waendeshaji wake kutokuwa na elimu ya udereva na sharia za barabara. Pia, vijana wengi wanapfanya shughuli hizi wako chini ya umri unaotakiwa au kuruhusiwa kuendesha vyombo vya moto kisheria na asilimia kubwa hawaja hudhuria mafunzo yeyote ya udereva. Hili limikuwa tatizo kubwa na chimbuko la ajali nyingi barabarani zinazo sababishwa na bodaboda.
Kampuni kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi idara ya Usalama barabarani na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji  {NIT} inatarajia kutoa mafunzo kwa Wilaya za mkoa wa Dar es Salaam na Pwani. Mafunzo haya yatakuwa niya kivitendo zaidi na kuwasaidia wadau wao kuweza kupata lesini na kusajili vituo vya kuegesha bodaboda zao.
 Wadau mbalimbali wanakaribishwa  kwamaana ya wadhamini wa mafunzo hayo kwani hii ni fursa ya kuisaidia juhudi za serikali na jamii kwa ujumla ya kuokoa maisha ya Watanzania wenzetu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List