Abdel-Fattah al-Sisi rais mpya wa Misri

Aliyekuwa mkuu wa jeshi nchini Misri , Abdel-Fattah al-Sisi, ndiye Rais mpya wa Misri baada ya kushinda uchaguzi mkuu uliofanyika wiki hii.
Vyombo vya habari vya kitaifa nchini Misri vinasema matokeo ya mapema yanaonyesha kwamba amejinyakulia zaidi ya asilimia 96 ya kura hizo.
Muslim Brotherhood na makundi mengine yaliususia uchaguzi huo na idadi ya waliojitokeza kupiga kura inakadiriwa kuwa chini ya asilimia 45.
Hii ni licha ya kuongezwa siku ya kupiga kura, kutangazwa siku ya kitaifa ya mapumziko na hata pia kutolewa usafiri wa bure kuwapeleka wananchi kupiga kura.
Sisi alimng'oa mamlakani aliyekuwa Rais Mohammed Morsi ambaye alikuwa Rais wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia nchini Misri.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List