WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII YAPANGA MIKAKATI YA KUBORESHA MAZINGIRA



Picha ya Pamoja ya Semina ya siku moja ya Makatibu tawala Mikoa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Charles Pallangyo

Dar es salaam

KATIBU MKUU wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Charles Pallangyo,
emesema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha inamaliza tatizo la taka
ngumu mijini  na vitongoji vyake.
Akizungumza katika semina ya siku moja ya MakatibuTawala wa  Mikoa
iliyofanyika katika Hoteli ya  jijini Dar Es Salaam,Pallangyo alisema,
Serikali imejipanga kumaliza tatizo hilo kuanzia katika ngazi ya
serikalii za mitaa hadi Mkoa.

 katika kampeni ya kumaliza tatizo la uchafu, hususani  katika miji,
kwani taka ngumu limekuwa tatizo sugu, hivyo tunafanya mikakati
mikubwa kuelekeza nguvu kuanzia  ngazi ya jamii hadi juu ngazi za juu

Aidha Katibu Mkuu huyo alisema, lengo la kuandaa semina hiyo ni
kupanga mikakati ya kuhakikisha mazingira ya usafi yanazingatiwa,
katika jamii ili kuhepukana na vifo vinavyotokana na  magonjwa ya
milipuko katibu mkuu wizara ya afya na ustawi wa jamii Charles pallagyo

Eliya Ntandu katibu tawala mkoa wa morogoro amesema lengo la serikali
ni kushirikiana pamoja na wanachi, secta binafsi,pamoja na wakandarasi,
kuzibiti mazingira na utupaji ovyo taka ngumu ambapo usimamizi huo
utasimamiwa na makatibu tawala wa kila mkoa

Wadau wa mazingira nchini pamoja na makatibu kutoka mikoa mbalimbali
waliudhuria semina hiyo wakisema kuwa nchini kumekuwa na tatizo kubwa
la usafi wa mazingira hivi sasa wizara imejipanga na kuweka mikakati
bora  ya udhibiti na uchafuzi wa mazingira kwa kushirikisha  wananchi

Pamoja na jitihada za serikari kupambana na usafi wa mazingira
wamebaini ipo haja  ya kushirikisha wananchi  pamoja na kutoa elimu ya
usafi wa mazingira ili kuepusha vifo na magonjwa ya mlipukoyanayotokana na uchafu.                                                                                 
                              
                           Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Charles Pallangyo



Mdau wa afya akichangia mada jinsi ya kuboresha usafi wa mazingira

ROBERT NTALENGA(mkurugenzi mwezeshaji wa Baraza la Mazingira Tanzania)

 Picha ya Pamoja ya Semina ya siku moja ya Makatibu tawala Mikoa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Charles Pallangyo




Eliya Ntandu katibu tawala mkoa wa morogoro

Wakiwa wanasikiliza maelezo kwa Makini ndani ya Semina.

mwisho
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List