SERIKALI ITATUMIA ZAIDI YA BILIONI 1.5 KWA UJENZI WA BWAWA KUBWA KISARAWE

Serikali itatumia zaidi ya bilion 1.5 kwa ujenzi wa bwawa kubwa la kuhifadhia maji ya mvua.hali hiyo imetokana na ardhi kuwa na madini mengi yaliyotokana na uchafuzi wa mazingira ambao umesababisha kutopata maji ardhini ambapo vikichimbwa visima baada ya muda vinakauka au wakati mwengine maji yanapatikana na madini mengi ya chumvi.

Kutokana na hali hiyo Serikali imeamua kuchimba bwawa kubwa litakalo tumika kuhifadhi maji yatakayotumika kijiji cha Chole na Kwale ila jumla vijiji 28 Vyote vitakuwa vimepata ufumbuzi wa changamoto ya maji kutokana na miradi iliyoandaliwa na Serikali.

Naibu Waziri wa Maji Mh.Amos Makala amesema wakandarasi wote watakaoshindwa kukabidhi mradi kwa wakati au kuhujumu mradi kwa ujenzi usio na kiwango watachukuliwa hatua za kisheria bila kuangalia ni nani au hata kufunga vibali vya kazi.

Mbunge wa jimbo la kisarawe Mh.Seleman Jaffu amewataka wanaanchi wawe na subira ya kusubiri utekelezaji wa miradi kwa kuwa mda si mrefu itatekelezeka na kutatua shida kubwa ya maji.

Uchimbaji wa bwawa kubwa ukiendelea Kisarawe

Naibu waziri wa maji Mh.Amos Makala na Mbunge wa Kisalawe Mh.Seleman Jaffu wakiwa na wataalamu wa maji wakipata maelezo ya ujenzi wa bwawa hilo.

Uchimbaji wa bwawa kubwa ukiendelea Kisarawe

Naibu waziri wa maji Mh.Amos Makala akimtwisha mwananchi maji wakati wa uzinduzi wa maji

Naibu waziri wa maji Mh.Amos Makala akizindua mradi wa maji ya kisima kirefu

Naibu waziri wa maji Mh.Amos Makala

 Mbunge wa Kisalawe Mh.Seleman Jaffu

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List