RAIS SHIRIKISHO LA FILAMU TAFF AMUUNGA MKONO STEVE NYERERE




IKIWA ni chache tu kupita tangu aliyekuwa Rais wa Bongo Movie Steve Mengele ‘ Steve Nyerere’ kutangaza kung’atuka kwenye wadhifa huo ,Rais wa  Shirikisho la Filamu nchini (TAFF),Simon Mwakifwamba amemuunga mkono kwa uamuzi huo.

Mwakifwamba akizungumza na Tanzania Daima jana alisemas kwamba uamuzi wa Steve ni wa busara  na anapaswa kupongezwa hadi hapo alipowafikisha Bongomovie inatosha.

“Binafsi mwishoni mwa wiki nilikiwa miongoni mwa watu waliomshauri afanye hivyo kwani hiyo ndiyo Bongomovie ambayo inatawaliwa na majungu kwakila kiongozi” alisema Mwakifwamba .

“Mimi nilimwambia steve Ijumaa iliyopita kwamba unaweza kulijenga jina lako kwa miaka 15 lakini ikifika mahali unaona majungu yamezidi na ili kuachana nayo bwaga manyanga waachie Bongomovie yao hao wanaoona ni rahisi kuongoza ili waone kama uongozi ni lelemama” alisema.

 Steve Nyerere alitangaza kujiuzulu  wadhifa huo  Ijumaa iliyopita kutokana na  kukithiri kwa majungu  ndani ya klabu hiyo ikiwa ni pamoja na kutoaminiana kwa hali na mali.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam Nyerere ambaye  ni msanii wa kucheza filamu pia mbobevu katika kuchekesha hasa kwenye kuiigiza sauti ya hayati baba wa Taifa na Rais wa Kwanza wa Tanzania  hayati Julius Nyerere ambako ndiko kuliko mpa umaarufu huo hadi hivi sasa.

“Kikubwa kilichonifanya nikimbie uongozi huu  ni kutokana na  mlolongo wa migogoro kila kunapokucha, kwani imekuwa ni kama jambo la kawaida kwa wasanii wa Bongomovie kila mara baada ya kumalizika shughuli fulani kama misiba , mkialikwa mahali  hata kwenye khitma za kuwaombea marehemu wao wameeka mbele fedha utasikia kala Nyerere kala hela nimechoka.

 Hivi ni kiongozi gani ambaye atavumilia kuzushiwa  kashafa kila kunapokucha  huku kwa silimia kubwa zikiwa ni za uongo hasa la kusingiziwa kula fedha tuhuma ambazo hazina ukweli ndani yake” alisema Steve kwa masikitiko.

Aidha aliendelea kwa kusema kuwa anaona kama vile wasanii wenzake wanamtumia na kumwona kama jalala la kutupa lawama zao ambazo hazina tija  hivyo kwa kulinda heshima yake ambayo amaeitengeneza kwa muda mrefu na kulinda heshima ya marafiki zake  na viongozi ambao wamekuwa wakimsapoti kila kunapokucha katika kulisukuma gurudumu la maendeleo ya wasanii ameamua kuachia ili mwenye uwezo aje ashike usukani wake.

“Haya ni maisha rafikiangu  kwanini tugombee fito ilhali wote lengo ni moja tu kujenga sanaa ambayo imetoa ajira kwa vijana wengi nchini, mimi ni baba wa familia hivyo nimechoka kuona kila siku nakashifika bila sababu za msingi acha sasa nikihangaika nitakachokipata nitagawana na familia yangu mke wangu na watoto wangu na watu wengine ambao watakuwa wakihitaji msaada wangu ”alisema Nyerere.

Uamuzi wa Nyerere kubwaga manyanga Bongomovie umekuja siku chache baada ya kufanikisha uzinduzi  wa filamu ya ‘Mateso yangu ughaibuni’  iliyorekodiwa nchini Uingereza  na kusimamiwa na Kampuni ya Didas Entertainment.

“Nimefikia uamuzi huu kwa roho safi wasije kuniua na presha za hovyohovyo hivyo maisha yangu yataendelea nje ya Bongomovie na cheo cha Urais” anamalizia.

Nyerere aliingia madarakani kwa kishindo mapema mwaka huu katika uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List