Mamlaka ya mapato nchini TRA imekabidhi  vifaa mbalimbali  kwa hospitali kuu ya mnazi mmoja iliyopo wilaya ya mjini hapa Zanzibar

Akikabidhi msaada huo kwa uongozi wa Hospitali hiyo Richard M Kayombo mkurugenzi wa huduma na Elimu kwa mlipa kodi amesema TRA kila mwaka imekuwa ikitoa misaada katika maadhimisho ya wiki ya mlipa kodi.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na magodoro 100,shuka 100,pashet screen 10 na oxygen set 3 ambapo vifaa vyote vimegharimu jumla ya shilingi milioni 20

Akipokea vifaa hivyo Dr Msafiri Marijani mkuu wa idara ya uchunguzi katika hospitali ya hiyo ameishukuru TRA kwa msaada huo na kusema kuwa hospitali hiyo bado ina changamoto nyingi kutokana na ufinyu wa bajeti,na kuziomba taasisi nyengine kuiga mfano wa TRA.

Aidha Kayombo amefahamisha kuwa mwaka huu wa 2014 TRA inafanya maadhimisho ya nane na tayari wamekabidhi madawati kwa shule kadhaa jijini  Dar es Salaam na kushiriki usafi katika hospitali ya Wilaya ya Temeke.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla hiyo Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi TRA makao makuu amesema TRAnchini ilianza rasmi mwaka 1996 ambapo kwa kipindi hicho makusanyo ya mwaka yalikuwa shilingi bilioni 35 na makusanyo yamefikia kiasi cha shilingi bilioni 900 kwa mwaka wa 2013/14.

Mkurugenzi huyo pia amewataka wafanyabiashara na wananchi wote nchini kuzingatia kulipa kodi ili kuinua uchumi wa taifa,pia amewataka watumiaji wa bidhaa kudai risiti ili kuhakikisha kuwa wafanyabiashara hawakwepi kodi.

Kilele cha wiki ya mlipa kodi kitafikiwa siku ya tarehe ambapo wafanyabiashara wanaolipa kodi bila shuruti watatangazwa hadharani na kutunukiwa vyeti maalumu na TRA.



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List