Breaking News! Jaji Werema aachia ngazi



http://2.bp.blogspot.com/-HfIVzV9HEPE/Uq2Qh28re9I/AAAAAAAALfk/iZ76iAX0yLA/s640/1.png
jaji Werema aliyetangaza kuachia ngazi mwenyewe

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema ametangaza kujiuzulu nafasi yake hiyo.
Habari hizo zinasema Jaji Werema mmoja wa vigogo wanaotuhumiwa kuhusika na sakata la uchotwaji wa fedha za Akaunti za Tegeta Escrow zipatazo zaidi ya Sh Mil 300.
Kwa mujibu wa taarifa hizo zinasema kuwa Jaji Werema ameamua kujiuzulu mwenyewe kwa hiari yake na kwamba Rais Jakaya Kikwete ameafikiana na maamuzi hayo na kumshukuru kwa ujtendaji wake na kumtakia kila la heri katika maisha yake mapya.
Hata hivyo taarifa hizo zinasema kuwa, maamuzi hayo yamekuja baada ya shinikizo kubwa ambalo limekuwa likitolewa kila pembe ya nchi kwa Rais JK kuwawajibisha wote waliotajwa kwenye mapendekezo nane ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kuhusiana na sakata hilo ambalo limeitia doa Tanzania mbele ya nchi wahisani.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List