V Persie anyimwa haki za kupiga Penalti

 

V Persie anyimwa haki za kupiga Penalti

  • Saa 7 zilizopita
Louis Van Gaal
Mkufunzi wa kilabu ya Manchester United Louis Van Gaal amempokonya mshambuliaji wa kilabu hiyo Robin Van Persie haki za kupiga mkwaju wa penalti baada ya kukosa mkwaju kama huo katika mechi dhidi West Brom.
Alipoulizwa iwapo Van Persie angeendelea kama mchezaji aliyeorodheshwa kupiga penalti kwa niaba ya kilabu hiyo alijibu ''hapana,amefika mwisho wake.Kila mara anarejelea makosa hayo hayo aliongezea''.
''Wayne Rooney pia amekosa mkwaju wa penalti na unapokosa mkwaju huo basi ujue utapiga foleni''.,aliongezea
Van Persie
Ushindi wa West Brom ulikuwa matokeo mabaya kwa upande wa Manachester United kwa mara ya tatu mfululizo.
Van Persie mwenye umri wa miaka 31 alikuwa na fursa ya kusawazisha kufuatia bao la Chris Brunty kunako dakika ya 63 baada ya refa Anthony Taylor kumpata na Saido Berahino na makosa ya kuunawa mpira katika eneo la hatari.

 

 

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List