Nabii Paul Bendera wa kanisa la ufunuo ambaye alitabiri
mapema ushindi wa Dokta John Pombe Magufuli kwa nafasi ya Urais ametabibiri Watanzania watajarajie
Mababiliko makubwa katika Serikali mpya baada ya Rais Mpya mteule kuapishwa.
Nabii Bandera amezungumza hayo katika mkutano wa waandishi
wa habari jijini Dar es salaam,kukamilisha utabiri wake wa Uchaguzi mkuu wa
Rasi,Wabunge na Madiwani.
Katika mkutano na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali Mwandishi wa
Blog alipata nafsi ya kujua matarajio ya Nabii kwa Rais Mpya.
Akijibu swali hilo amesema watanzania watarajie mabadiriko
makubwa katika Serikali kuu Mpya na
akijibu kuhusu madai ya Kuibiwa kwa kura kwa Upinzani amesema Hakuna mtu yoyote
anayeweza kuipora haki ya MUNGU.
Alimalizia kwa kusema yeye sio mfuasi wa Siasa ila ametabiri
kutokana na Maono ya MUNGU na ametabiri wabunge na madiwani kutoka vyama
mbalimbali vya siasa.Nabii Bendera alitoa utabari wake Septemba Nane mwaka
huu,kwamba Dokta Magufuli atashinda nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu
uliofanyika oktoba 25 pia mwaka 2015 pia alitabili vitatokea vifo vya
kushtukiza vya wanasiasa kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu.
0 comments:
Chapisha Maoni