UPUNGUFU WA WALIMU

Shule ya Msingi Jeshi la wokovu ya jijini Dar es salaam,inayotoa Elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum,ina upungufu wa walimu wa Sayansi na hisabati kwa muda mrefu hivyo imeiomba serikali kuwasaidia  watoto wenye uhitaji ili wapate elimu.
Hayo yamesemwa wakati wa kupokea msaada wa Baiskeli na Fimbo kwa watoto wenye ulemavu wa macho na miguu Kutoka kwa taasisi ya Mohamed Punjan Foundation ya nchini CANADA.
Meja Wilson Chacha ni Mkurugenzi wa shule ya Jeshi la wakovu ameshukuru msaada huo kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watoto wanaosoma katika shule hiyo huku wazazi wao wakiwa hawana uwezo.
Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Mohamedi Punjan amesema wameguswa na matatizo mbalimbali ya watoto wenye ulemavu na kuamua kufika Tanzania kwa ajili ya kutoa msaada katika taasisi hiyo.
Taasisi ya Mohammed Punjan Foundation ya Kutoka nchi ya CANADA wamefika Tanzania kwa lengo la kusaidia watoto wenye ulemavu wa miguu na kuwapa Baiskeri za kutembelea pamoja na fimbo.Pia wametoa msaada kwa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi kwa kuwapa msaada wa zaidi ya milioni 60.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List