ZAHANATI UMEME

Wananchi wa mtaa virobo kata ya Chanika wamekuwa wakipata Huduma ya matibabu kwa wakati wa usiku kwa kutumia mwanga wa simu kutokana na kukosekana kwa umeme katika Zahanati ya Yangwe iliyopo wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam.
Kutokana na hali hiyo wadau wameombwa kusaidia kupatikana kwa umeme wa TANESCO kutokana na umeme uliopo wa jua kutokidhi ya  mahitaji hospital hiyo.
Daktari wa zahanati ya Yongwe  Ally  Malika ameshukuru chama cha mapinduzi Wilaya ya Ilala kwa kuwapatia umeme wa sola.
Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala ndugu Kafuge Joel amewataka wananchi kuwa na subira sababu chama cha mapinduzi kinataka kuendelea kutekeleza Ilani kwa vitendo.Naye Mwenyekiti wa Mtaa akiongea amesema Serikali itahakikisha inaleta umeme katika Zahanati hiyo.
Licha ya kuwa Zahanati hiyo imesaidiwa umeme ila bado lina changamoto ya maji na upungufu wa wahudumu.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List