Mzee wa upako akemea njia zinazotumiwa na mkuu wa mkoa kwenye vita dhidi ya dawa za kulevya.

Mchungaji Lusekelo amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachofanyika kupitia ukurasa wa facebook wa EATV kila Jumatano kuanzia saa nane mchana hadi saa kumi jioni.

Lusekelo anadai kuwa mwaka 1997 alituhumiwa kuuza dawa za kulevya lakini anakiri wazi kuwa polisi wa kipindi kile walikuwa ni wastaraabu kwani waliamuandikia samansi na kumuomba kufika kituo cha polisi kutoa maelezo, hivyo anasema alifika na kutoa maelezo yake lakini taarifa hiyo ilivuja mtaani jambo lililopelekea watu kumtenga.
“Mimi ni mhanga wa dawa za kulevya mwaka 1997 nilituhumiwa kuwa nauza madawa, lakini wale askari walikuwa wastaarabu, waliniandikia samasi nikafika kutoa maelezo yangu, lakini baadaye niliwaambia kuwa wao ni polisi wafanye uchunguzi wao, walifanya uchunguzi na kugundua mimi sihusiki, watu walifuatilia na kugundua siyo kweli, na kila mtu akajitoa kwenye, ilionekana kuwa ni wivu tu, ila mbaya zaidi ile taarifa kuwa niliitwa polisi kwa madawa ya kulevya ilivuja, hadi wachungaji wenzangu walininyanyapaa, nikivaa suti au nikiendesha gari kila anajua ni pesa za madawa” alisema Mzee wa Upako

Paul Makonda – Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye kwa takriban wiki moja amekuw akitaja watu mbalimbali wanaodaiwa kuhusika na dawa za kulevya ambapo katika majina 65 aliyotaja leo, limo jina la Mchungaji Josephat Gwajima
Mzee wa Upako ameshauri vita ya dawa za kulevya kwa watu wanaotuhumiwa ni bora viongozi wangetumia njia za kipolisi kuwataka kufika polisi kwani kutumia njia ya magazeti inaweza kushusha heshima ya baadhi ya watu ambayo wameijenga kwa miaka mingi.
“Mimi kutokana na tuhuma zangu kuvuja kuwa niliitwa polisi kwa madawa ya kulevya niliishi miaka saba watu wananinyayapaa, tena hiyo ni tuhuma tu. Imenichukua miaka saba kusafisha jina, nimekuja kuanza kusafisha jina mwaka 2005 hivi”
Amesema yeye binafsi anachukia sana dawa za kulevya kutokana na madhara yake kwa jamii, hivyo hawezi kuthubutu kujihusisha nazo wala hawezi kuunga mkono watu wanaofanya shughuli hizo kwa kuwa dawa za kulevya zinaua kizazi cha maendeleo na taifa kwa ujumla.
Baadhi ya watu katika kipindi hicho walitaka maoni yake kuhusu Mchungaji Josephat Gwajima kuhusishwa na dawa za kulevya ambapo Lusekelo alisema hawezi kulizungumzia suala hilo na kutaka watu wasubiri hadi mwisho wake ufike ndipo na yeye anaweza kusema lolote.
Mchungaji Josephati Gwajima
Pia alishauri watu wanaowataja viongozi waliojijenga kwa muda mrefu kama Mchungaji gwajima wanapaswa kuwa na uhakika na ushahidi mkubwa usio na shaka, maana ikija kubainika kuwa siyo kweli, litakuwa ni kazi ngumu kwa viongozi hao kujisafisha kama ilivyomtokea yeye mwaka 1997.
“Kama kweli kuna wachungaji wanajihusisha au wanadhaniwa kuhusika kwenye madawa ya kulevya nashauri tungetumia njia ya wao kuitwa kwa samasi, tunapaswa kuwa makini katika hili kwani kujenga heshima ni kitu kikubwa, njia ya kuwaita watuhumiwa kwa njia ya magazeti si jambo nzuri kabisaa” amesisitiza Mzee wa Upako
Kwa wale waliotaka kujua jinsi anavyomuelewa Mchungaji Gwajima, Lusekelo amesema kuwa Gwajima ni rafiki yake, na wanaheshimiana sana.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List