PADRE JOEL ELIA KUSUPA AONGOZA MISA TAKATIFU YA KUSHEREKEA KUZALIWA KWA YESU.


Wakristo  wote duniani wakiadhimisha siku ya kuzaliwa Mtoto Yesu Bethelemu wametakiwa kusherehekea kwa Upendo na Amani.

Baba Padre Joel Elia Kusupa wa Kanisa la Angrikana st Agnes lililopo Yombo Vituka wilaya Temeke Jijini Dar es salaam akiendesha ibada hiyo amesema Bwana Yesu Kristo amezaliwa katika Mazingira Magumu.Amezaliwa katika zizi la Ngombe sehemu wanyama kukuwepo vinyesi vya Wanyama amezaliwa katika Mazingira Magumu kwa maisha ya binadamu ya wasiwasi na Mashaka lakini Mungu yuko pamoja nao kumlinda na  kumtetea,amesema binadamu wanapokuwa na magumu au matatizo mara nyingi Mungu hutokea na kutoa suluhu.



Kwa watu wenye matatizo uwapa nguvu,kuwafariji wanapo mtegemea Mungu. Umasikini si mpango wa Mungu hivyo unatakiwa kutegemea na kumwamini MUNGU. 



Ujumbe wa Yesu Kristo ni Amani Upendo na Imani utowa katika hofu mahangaiko na kukuweka katika furaha. Maadhimisho hayo ya Sikukuu ya Krimas yalienda sambamba na kuwazadia zawadi akina mama Wajane na Watoto Yatima na Watoto wadogo walibatizwa katika Kanisa la Mtakatifu Sat Agnes Yombo Vituka jijini Dar es salaam .


 



Share on Google Plus

About SDM PRODUCTION MEDIA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List