MATUKIO KATIKA PICHA KUTOKA BUNGENI DODOMA

 Baadhi ya Maofisa Habari  Mawasiliano wa Wizara za Serikali,  wakielekea katika Ukumbi wa Mkutano wa Bunge mjini Dodoma, leo. Maafisa hao wamefanya ziara  Bungeni hapo ili kuona  shughuli za Bunge.
 Baadhi ya Maafisa Habari Mawasiliano Serikalini wakiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene (wa nne kutoka kushoto mstari wa mbele). Wakiwa ndani ya ukumbi wa Bunge leo kuangalia shughuli za Bunge mjini Dodoma.
 Baadhi ya Maafisa Habari Mawasiliano Serikalini wakiwa ndani ya ukumbi wa Bunge.
 Naibu Waziri, Ofisi ya  Waziri Mkuu (TAMISEMI) Aggrey Mwanri akiwakilisha hati mezani kuhusu Taarifa ya  Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa na Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha,2010/2011.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Pereira Silima  akiwasilisha azimio la Bunge la Kujiunga na Mkataba wa Kimataifa wa Kuzuia Vitendo vya Ugaidi wa Kutumia Nyuklia. Azimio hilo limeungwa mkono leo  katika mkutano wa kumi kikao cha nane.
 Waziri wa  Elimu na Mafunzo ya Ufundi Shukuru Kawambwa (kulia) akiongea  na James Mbatia (Kushoto)- katika viwanja vya Bunge leo. Baada ya   Spika Anne Makinda(hayupo pichani) kutangaza rasmi Mitala ya  Elimu inayotumika ni halali na ipo. (Pichani katikati) ni   Charles Mwijage (Muleba Kaskazini).
 Mwenyekiti wa Bunge Mussa Zungu Azzan akifafanua kanuni mbalimbali Bungeni leo.

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe(kushoto) akiongea na  Joshua Nassari(Arumeru Mashariki) ndani  ya ukumbi  wa Bunge. Picha  Mwanakombo Jumaa- MAELEZO.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List