Chama cha Alliance for Democratic Change ADC kimempitisha Lutayosa Yemba kuwa mgombea wa Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Huku Mwenyekiti wa chama hicho Said Miraji Abdallah akiteuliwa kuwa mgombea mwenza,ambapo kwa upande wa Zanzibar utawakilishwa na Hamad Rashid Mohamed aliyekuwa Mbunge wa Wawi.
Hatua hiyo imefuatia baada ya Wajumbe wa chama hicho kuwathibitisha wagombea hao kwenye Mkutano Mkuu wa Chama,ambapo vipaumbele kwenye Irani ya chama vikiwa ni kusimamia haki,Usawa,Utu na kuilinda amani ya nchi.
Akifungua mkutano Mwenyekiti wa ADC Taifa Said Miraj Abdalah amesema ili maadhimio hayo yatimie watahakikisha wanatoa Elimu kwa mpiga kura ili aweze kuchagua mtu sahihi atakayeleta maendeleo ya nchi na siyo kuangalia chama.
Kwa upande wake Mgombea urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Chief Lutayosa Yembe amesema sekta ya afya na maji ndiyo vipaumbele vyake vya kwanza endapo atapata nafasi hiyo kutokana na umuhimu wa huduma hizo.Naye Mgombea urais kwa Zanzibar kupitia chama hicho amezungumzia suala la uchumi kwa namna ya kipekee katika kuleta mabadiriko.
Hatua ya chama hicho cha ADC kuwapitisha wagombea urais kwa Tanzania bara na Zanzibar ni miongoni mwa michakato inayoendelea kwa baadhi ya vyama vingine vya siasa wakati ikiwa inaelekea katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika October 25 mwaka huu.
- Blogger Comment
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Inaendeshwa na Blogger.
About Me
Wanaofuata
TANGAZO
My Blog List
-
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masum...Miaka 5 iliyopita
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye kwa sasa anamnowa bondia Sunday Kiwale 'Moro Best' kwa aj...Miaka 5 iliyopita
-
BONDIA MAKUBI ATAMBA KUMPIGA ABDALLAH MA MOROGORO OKTOBA 4 KATIKA UKUMBI WA 361 MWENGE - Na Mwandishi wetu Bondia Ibrahim Makubi yupo kambini kwa ajili ya mazoezi yake ya kumkabili bondia abdallah kingolwira wa ( morogoro ) katika pambano l...Miaka 5 iliyopita
-
JUMA CHOKI AJIANDAA NA MASHINDANO YA KING OF THE RING JULAI 28 - Bondia Ibrahimu Makubi kushoto akioneshana umwamba na Juma Choki wakati wa Mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Super D iliyopo shule ya Uhuru Kariakoo...Miaka 6 iliyopita
-
0 comments:
Chapisha Maoni