BARAZA LA WAZEE MKOA WA DAR ES SALAAM WATOA BARAKA KWA DKT JOHN POMBE MAGUFULI

Rais Jakaya Kikwete amesema hakuana mgombea ama mwana siasa anayeweza kuwanunua watanzania wote,ili wamuunge mkono kwenye juhudi zake za kushika wadhifa anaowania huku wakimnadi mgombea wa chama cha mapinduzi.,Dkt John magufuli kuwa ni kiongozi mwenye uwezo na uzowefu mkubwa

Aidha Rais Kikwete amewetaka wana ccm kujitokeza kwa wingi kumpigia kura mgombea wao ili aweze kushinda na kuendeleza yale ambayo tayari serikali ya awamu ya nne ilioanza kuyatekeleza.

Alipokuwa akizungumza na wazee wa ccm wa mkoa wa dar es salaam rais Kikwete amesema wapo baadhi ya wana siasa wanaotanguliza fedha ili kuwanunua watanzania wawaunge mkono kwenye nafasi wanazogombea ambapo amesema hata wakifanya hivyobado hawatofanikiwa kuwanunua watanzania wote.

Mgombea wa Urais kpitia chama hicho Dkt John Pombe Magufuli aliyeambatana na Rais Kikwete yeye kwa upande wake pamoja na kuwashukuru wananchi kwa kumpa furs hiyo huku akiwaidi kuongoza nchi kwa kuzingatia kwamba Tanzania ni Moja.

Rais kikwete aliongozana pia na Mgombea mweza wa Urais CCM Samia Suluhu,Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es salaam Ramadhani Madabida na viongozi wengine wa Chama na Serikali na Lengo kubwa likiwa ni kuwaomba wazee hao kumuunga mkono mgombea wa sasa Dkt Magufuli katika safari yake.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List