SOKO LA KARIAKOO LIKO HATARINI KUPOTEZA BIDHAA MUHIMU

Wafanya biashara wa soko kuu la kariakoo jijini dar es salaam wameiomba serikali kuruhusu magari ya mizigo kufika katika soko hilo kwani wanaathirika kiuchumi kutokana na kukosekana kwa bidhaa.

Wafanya biashaa hao wamelalamikia Manispaa ya Ilala kwa kupandisha ada ya vibali na masharti ya muda wa kuingia katika soko hilo,Mambo ambayo yamesababisha wakulima kushindwa kufikisha bidhaa zao katika soko hilo,Na baadala yake kupeleka katika masoko mengine.

Meneja wa soko hilo Florens Saiya amesema licha ya changamoto kuwa nyingi katika eneo hilo la soko lakini mapato yamekuwa yakiongezeka  na tatizo la kukatika umeme limepatiwa ufumbuzi kwa ununuzi wa jeneleta kubwa la kuzalisha nishati hiyo ya umeme.

Afisa Biashara wa manispaa ya Ilala hakupatikana kuzungumzia lalamiko hilo la wafanya biashara wa soko hilo.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List