Wanawake wamelalamikia ubaguzi katika uteuzi wa wagombea kuwania nafasi za ubunge na udiwani Tanzania.

Wanawake wamelalamikia ubaguzi katika uteuzi wa wagombea kuwania nafasi mbalimbali za uongozi Tanzania.Wanawake hao wamelalamika katika mkutano wa wanawake kwamba vyama vyote vya siasa vimetoa fursa ndogo kwa wanawake nchini kushiriki katika uchaguzi huo.

Kwa upande wa CCM wanawake mamelalamikia kura za maoni kuwa zilitawaliwa na rushwa na vikao vya maamuzi vilishindwa kuwatetea wanawake walionyesha  uwezo mzuri wa kisiasa na uongozi.

Kwa upande wa UKAWA wamelalamikia muungano huo kushindwa kutoa kabisa fursa kwa wanawake kutokana na utaratibu wa kugawanywa majimbo kwa vyama vinvyounda UKAWA,mfumo huo ambao umeonekana ni mbovu na kutoa fursa chache kwa wanawake,Pia wamelalamikia chama cha CUF kwa kushindwa kutoa fursa kwa wanawake .

Wanawake hao wamepaza sauti kwa upande wa Tanzania visiwani kwa kuonyesha mwitikio mdogo kwa wanawake walionyesha nia ya kuwa viongozi na kushauri mshikamano ili kumkomboa Mwanamke wa Tanzania.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List