Rooney awachanganya mashabiki Dar, Mwakyembe atoa neno
Hatimaye mapema leo timu ya Everton imewasili jijini Dar es Salaam kwa lengo la kushiriki mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya Gor Mahia ya nchini Kenya.
Wakati timu hiyo ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), wachezaji wote walishuka kwenye ndege yao binafsi na kuelekea katika basi lao maalum huku wakipita kila mmoja kumshika mkono mwenyeji wao, Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni, Dk. Harrison Mwakyembe. Lakini mchezaji mpya wa klabu hiyo, Wayne Rooney alionekana kuwachanganya zaidi mashabiki waliofika uwanjani hapo.
Rooney ambaye alikuwa wa mwisho kushuka kwenye ndege hiyo alionekana kushangiliwa zaidi na mashabiki ambao walisikika wakimpa ujumbe mbalimbali, huku wengi wakimtaka ageuka angalau awapungie mkono.
Hata hivyo, mchezaji huyo alitulia kama anazisikia kelele za mashabiki wake akiwa Goodison Park akiambaa taratibu na mpira. Mchezaji huyo aliyeiahama Manchester Utd hivi karibuni aliendelea kutembea, kumshika mkono Dk. Mwakyembe na kuelekea kwenye gari.
Akizungumza muda mfupi baada ya wachezaji hao kuingia kwenye basi lao, Waziri Mwakyembe aliwataka mashabiki wote walioko uwanjani na majumbani kuendelea kuwa watulivu na kuhudhuria mechi itakayofanyika kesho katika Uwanja wa Taifa wa Dar es Salaam.
“Hii ni timu kubwa na Tanzania inafarijika sana kwa ujio huu. Niwaambieni tu Watanzania hata ninyi waandishi wa habari, ulinzi umeimarishwa na katika mazoezi yao hataruhusiwa mtu yoyote asiyehusika kwenda,” alisema Dk. Mwakyembe.
Timu ya Everton iliwasili JNIA majira ya saa 2 na dakika 39 na kuelekea hotelini majira ya saa 3 na dakika 10.
- Blogger Comment
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Inaendeshwa na Blogger.
About Me
Wanaofuata
TANGAZO
My Blog List
-
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masum...Miaka 5 iliyopita
-
SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA - Na Mwandishi Wetu KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye kwa sasa anamnowa bondia Sunday Kiwale 'Moro Best' kwa aj...Miaka 5 iliyopita
-
BONDIA MAKUBI ATAMBA KUMPIGA ABDALLAH MA MOROGORO OKTOBA 4 KATIKA UKUMBI WA 361 MWENGE - Na Mwandishi wetu Bondia Ibrahim Makubi yupo kambini kwa ajili ya mazoezi yake ya kumkabili bondia abdallah kingolwira wa ( morogoro ) katika pambano l...Miaka 5 iliyopita
-
JUMA CHOKI AJIANDAA NA MASHINDANO YA KING OF THE RING JULAI 28 - Bondia Ibrahimu Makubi kushoto akioneshana umwamba na Juma Choki wakati wa Mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Super D iliyopo shule ya Uhuru Kariakoo...Miaka 5 iliyopita
-
0 comments:
Chapisha Maoni