Hivi karibuni watu wameshuhudia bint Mariamu Juma wa Kijitonyama jijini Dar es salaam akizawadiwa kila kitu cha nyumbani pamoja na fenicha za Masofa kabati kubwa la nguo,Vyombo,friji na mziki mkubwa baada ya kufunga ndoa. Mama mzazi wa bint huyo amesema hiyo ni tamaduni za watu wa Pwani unatakiwa unapomuozesha mtoto unamzawadia kila kitu ili asiende pata tabu baadaye.
Mama huyo anaye julikana kama Esta Yahuo alimaarufu bibiTajiri wa mtaa Kongo akishirikiana na wafanyabiashara wa Vijora,amesema wametowa Viwanja viwili kutoka katika umoja wao wa wafanyabiashara wa Machinga Kongo Dar es salaam wa kuwezeshana wakati wa Shughuli za furaha.Umoja huo una utaratibu wa ukitunzwa unatakiwa nawe wakati hukifika wa uliyekutuza nawe unarudisha fadhila na kama uwenzi usiingie umoja huo.kuendeleza tamaduni za watu wa Pwani.
Yeye si mtu wa Pwani bali aliolewa na mtu wa pwani kwahiyo anawejengea watoto msingi wa mira za kwao.
0 comments:
Chapisha Maoni