MSECHU: VIDEO YA 'kIBUDU' NITAIFANYA KENYA




 Na Elizabeth John



HATIMAYE ngoma inayokwenda kwa jina la ‘Kibudu’ liyoimbwa na mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Peter Msechu, imeanza kutamba katika vituo mbalimbali vya redio kutokana na ujumbe wa mashairi yaliyomo ndani yake.

Mbali ya kutamba na kibao hicho, mkali huyo alishawahi kutamba na kibao chake cha ‘Relax’, ‘Kumbe’ ambavyo vilifanya vizuri zaidi mbali na kuwa na vibao vingi ambavyo vilimtambulisha katika tasnia ya muziki huo.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, Msechu alisema katika kazi hiyo kamshirikisha mkali wa muziki huo, Ally Nipishe na kwamba tayari imeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Alisema kibao hicho kakitengeneza katika studio ya Ufundi Production chini ya mtayarishaji wake mahiri, Fundi Samuel.
“Naomba mashabiki wangu wakipokee vizuri kibao hicho ambacho natarajia kukifanyia video yake Nairobi, Kenya,” alisema.


Msechu aliwataka mashabiki wake wakae mkao wa kula kwa ajili ya video hiyo ambayo anatarajia kuitoa mwinzoni mwa mwezi ujao ikiwa ni pamoja na nyimbo nyingine nyingi zinazofuata.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List