BREAKING NEEEWZ!!! BABA MZAZI WA WEMA SEPETU, BALOZI ISAAC SEPETU AFARIKI DUNIA



HABARI zilizotufikia hivi punde mtandao huu, zinasema kuwa, Baba Mzazi wa msanii wa Filam nchini na Miss Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu, Balozi Issac Abraham  Sepetu, amefariki Dunia asubuhi ya leo katika Hospitali ya TMJ Mikocheni jijini Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa.
Aidha imeelezwa kuwa, Balozi Sepetu alikuwa amelazwa katika hospital ya TMJ akitibiwa ugonjwa wa Kisukari na kiharusi uliokuwa ukimsumbua.
Hadi umauti unamkuta,Balozi Isaac Sepetu alikuwa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar.
Mtandao huu unaungana na waombolezaji wote wa Msiba huu na Mwenyezi Mungu, Aiweke Roho ya Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu, Mahala Pema Peponi .
-Amen-
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List