NDEGE 3 WAIBUKA NA SINGO MPYA





KUNDI jipya la muziki la Ndege 3, linaloundwa na wasanii watatu nyota wa muziki wa dansi nchini, limeibuka na kibao kingine kipya.

Wasanii wanaounda kundi hilo ni Khadija Mnoga (Kimobitel), Pauline Zongo na Joan Matovolwa.

Taarifa iliyotumwa na Khadija kwa blogu ya Liwazozito wiki hii, imeutaja wimbo huo kuwa ni Misukosuko.

Ndege 3wamerekodi wimbo huo kwa kushirikiana na repa machachari nchini, Grayson Semsekwa wa bendi ya Twanga Pepeta.

Khadija alisema tayari wamesharekodi audio ya wimbo huo na kuzisambaza kwenye vituo mbalimbali vya redio nchini.

Amesema kwa sasa wanajiandaa kurekodi video ya wimbo huo kabla ya kuisambaza kwenye vituo vya televisheni nchini.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List