Diwani kata ya Kibiti adai kurudishiwa gari la wagonjwa

 Diwani wa kata ya kibiti wilayani rufiji mkoani pwani Mh.Amidu Ungando  amemlalamikia mkuu wa mkoa Mh.Mwantumu Mahiza kwa kuhamisha gari la wagonjwa kutoka kituo cha afya kibiti  na kulipeleka kwenye zaanati ya nyamisati

Diwani huyo alidai kwamba gari hilo lilitolewa kama msada na taasisi ya afya..ya Ifakara (IHI) mnamo Mei 2 kwa lengo la kuwaudumua watu wengi ktoka kata mbali mbali za wilaya ya Rufiji..
.
"hili gari la wagonjwa lili tolewa kwa ajili ya kituo cha afya cha kibiti,inakuaje mkuu wa mkoa analipeleka kata nyingine tena kwenye zahanati? ninavyo vielelezo vya makabidhiano kutoka IHI ," ali lalamika Diwani Ungando mbele ya wananchi wake..

 Hata hivyo Mkuu wa mkoa wa pwani  Mh.Mwantumu Mahiza amesema uwamuzi wa kuamisha gari hilo,ulitokana na ukweli kwamba kituo hicho afya cha Kibiti tayari kina gari lingine hivyo serikali ilionelea ni vyema na Zahanati ya Nyamisati nayo ikapatagari la wagonjwa..

 "kata ya Nyamisati wanapata shida kubwa ya usafiri wa kuwafikisha wagonjwa kwenye zahanati na vituo mbalimbali vya afya,"alisema mkuu huyo wa mkoa.


  
Mwananchii wa kata ya Kibiti akilalamika kwa kata
yao kunyang'anywa gari la wagonjwa














Wananchi wa kata ya Kibiti wakimsikiliza diwani wao
(hayupo pichani)













Mkuu wa Mko wa pwani Mh.Mwantum Mahiza

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List