Wanajeshi washika doria mjini Bangkok

Wanajeshi walinda baadhi ya ofisi za serikali mjini Bangkok
Maelfu ya polisi pamoja na wanajeshi wamepelekwa katika mji mkuu wa Thailand Bangkok kwa jaribio la kuangamiza maandamano dhidi ya mapinduzi ya kijeshi ya mwezi jana.
Baadhi ya vituo vya treni pamoja na maduka ya jumla yamefungwa kutokana na maandamano hayo.
Mwandishi wa BBC mjini Bangkok amesema kuwa eneo la biashara katikati ya mji huo limesalia kuwa mahame baada ya jeshi kulifunga.
Siku ya ijumaa kiongozi wa jeshi Jenerali Prayuth Chan Ocha aliziambia pande pinzani kushirikiana na kuwacha maandamano ili kuleta maridhiano.
Katika hotuba hiyo kiongozi huyo amesema kuwa uchaguzi mpya hautaitishwa hadi baada ya mwaka mmoja.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List