Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
limepokea taarifa za kutolewa
wito bungeni wa kulitaka litumie tiketi za elektroniki katika kukusanya
mapato.
wito bungeni wa kulitaka litumie tiketi za elektroniki katika kukusanya
mapato.
Tunataka ieleweke wazi kwa umma wa Watanzania kuwa
si nia yetu
kuchelewesha matumizi ya uingiaji mpirani kwa tiketi za elektroniki. Ieleweke
kuwa mfumo wa kuingia kwenye mbuga, KCMC, mipakani ni tofauti na uingiaji
mpirani.
kuchelewesha matumizi ya uingiaji mpirani kwa tiketi za elektroniki. Ieleweke
kuwa mfumo wa kuingia kwenye mbuga, KCMC, mipakani ni tofauti na uingiaji
mpirani.
Katika mpira wa miguu wanaingia maelfu ya watu
katika kipindi kifupi. Kwa kuzingatia umuhimu wa kulinda usalama wa watazamaji
na miundombinu ya viwanja ndio maana tulisitisha matumizi ya tiketi za elektroniki
hadi tujihakikishie usalama wa matumizi yake.
Tunafanya jitihada kwa karibu na mzabuni benki ya
CRDB ili kuhakikisha mfumo huu unaanza kutumika mara moja.
Kwa niaba ya sekta ya michezo tunatoa wito kwa
Serikali kushusha au kuondoa kodi kubwa zinazotozwa kwenye vifaa vya michezo,
hasa vinavyotumiwa na watoto kuanzia umri wa miaka 6-12, ili watoto wetu waweze
kuvipata kirahisi toka kwa wazazi wao ili waweze kujifunza kucheza michezo
kisasa tangu wakiwa wadogo.
TAIFA STARS KUINGIA KAMBINI JUNI 11
Kikosi cha Taifa Stars kinaingia tena kambini Jumatano
(Juni 11 mwaka huu) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya raundi ya pili ya
michuano ya Afrika dhidi ya Msumbiji itakayochezwa Julai 20 mwaka huu jijini
Dar es Salaam.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwa
na kambi ya siku tatu jijini Dar es Salaam ikijumuisha wachezaji 28. Kwa mujibu
wa programu ya Kocha Mart Nooij, Stars itaingia tena kambini Juni 24 mwaka huu.
Wachezaji wanaotakiwa kuripoti kambini ni Deogratias
Munishi, Aishi Manula, Benedictor Tinoko, Kelvin Yondani, Said Moradi, Nadir
Haroub, Joram Nason, Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Edward Charles, Aggrey
Morris na Pato Ngonyani.
Wengine ni Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Amri Kiemba,
Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Said Juma, Haruna Chanongo, Himid Mao, Said Ndemla,
John Bocco, Simon Msuva, Kelvin Friday, Ramadhan Singano, Khamis Mcha, Mrisho
Ngasa na Mwegane Yeya.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF
Blogger Comment