Mwanaafa Mwinzago akipozi katika studio za Global TV Online.
Staa
 wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 Mwanaafa Mwizago 
kutoka Kanda ya Kusini Mkoa wa Mtwara akiwa ndani ya Studio za Kampuni 
ya Global Publishers Ltd wakati alipokwenda kufanyiwa Mahojiano na 
Wachapishaji wa Magazeti ya Uwazi, Risasi, Ijumaa na Ijumaa Wikiendi.
 Mara
 baada ya Kutua katika Ofisi za Kampuni ya Global Publishers Ambao ni 
Wachapishaji wa Magazeti Pendwa Hapa Nchini Mwanaafa alipata nafasi ya 
Kuongelea Namna ya Yeye alivyoweza Kuibuka Mshindi katika Shindano hilo 
Kubwa na La Kwanza Kufanyika Afrika Mashariki na Kati lijulikanalo kama 
Tanzania Movie Talents (TMT) huku akielezea Jinsi alivyoweza kupokea 
ushindi alioupata Mwishoni mwa Wiki katika Ukumbi wa Mlimani City Ambapo
 Fainali ya Shindano hilo Kubwa ilipofanyika na Yeye Kuibuka Kinara wa 
Shindano hilo kwa Mara ya Kwanza.
Shindano
 La Tanzania Movie Talents (TMT) limekuwa shindano la Kwanza na Kubwa 
Kufanyika kwa mara ya Kwanza Afrika MAshariki na Kati huku likiwa 
limejinyakulia Sifa na Umaarufu wa Hali ya Juu kutokana na Umahiri wa 
Uendeshaji wa Shindnao hilo ambapo Watanzania Wengi wamefurahishwa na 
Uendeshaji wake uliojikita katika Utendaji wa Haki ambapo Mshindi 
alipatikana kihalali.
Tanzania
 Movie Talents (TMT) imepelekea sasa kuwafanya baadhi ya Watanzania 
ambao waliokuwa wanajua kuwa shindano hili halitatenda haki basi Kuanzia
 sasa wamejionea kuwa TMT ipo kwaajili ya kutoa haki. TMT ni shindano 
ambalo  kiukweli Limefungua Njia Kwa Watanznaia Ambao wana vipaji lakini
 hawajapata nafasi ya Kuonekana.
Tanzania
 Movie Talents (TMT) limeendeshwa takribani Miezi Minne huku kukiwa na 
Changamoto Nyingi ambazo timu nzima ya Kampuni ya Proin Promotions Ltd 
ambayo ni waandaaji na waendeshaji wa Shindano hili Kubwa kujitahidi 
kutatua changamoto hizo ili kuhakikisha Shindano hilo linafanyika kwa 
Ustadi wa hali ya Juu na Utofauti.
Mbali
 na Zawadi hiyo kubwa aliyoshinda Mshindi wa TMT 2014 Mwanaafa Mwizago 
zawadi nyingine ambayo amepata Kutoka Kampuni ya Proin Promotions ni 
Kuwa Kampuni ya Proin itamsomesha Mwanaafa Mwizago katika Level Zote 
kwasababu kampuni inatambua Umuhimu wa Elimu Kwa Mtanzania. 
Sasa
 Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) limemalizika kwa Mshindi mmoja
 wapo kutoka kanda ya Kusini Mkoa wa Mtwara Mwanaafa Mwizago kuibuka 
Kidedea na Kujinyakulia Kitita Cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania 
huku washiriki wengi wote tisa waliofanikiwa kuingia hatua ya Fainali 
wakisubiri kucheza filamu ya Pamoja ambapo filamu hiyo itauzwa na 
Kusambazwa na Kampuni mahiri ya Utengenezaji na Uuzaji wa Filamu 
Tanzania ya Proin Promotions Ltd. 
0 comments:
Chapisha Maoni