TBL watoa msaada wa milioni ishirini kwa ajili ya uchimbaji wa kisima cha maji kituo cha afya cha Mbagala Roundtable Matenity Home Clinic

Kampuni ya Tbl imetoa msaada wa kuchimba Kisima   cha Maji safi na Salama katika Kituo cha Afya Mbagala Roundtable Matenity Home Clinic Kisima hicho kitaghalimu milioni 20 lengo kupunguza shida wanayopata wananchi pindi wanapofika kituo hicho kwa matibabu na kina mama kwa lengo la kujifungua.

Kituo hicho kimezidi kupanuka kutoa huduma ukilinganisha na hawali ambapo walikuwa wakitoa huduma kwa akina namama  na watoto na hivi ssa hutolewa huduma kwa jinsia zote kutokana na kuongezeka kwa wakazi wa maeneo hayo kuwa wengi baada ya majengo kuongezeka ya kuishi watu mbalimbali.

Kituo hicho hivi sasa kinatoa huduma zidi ya watu 500 kwa siku kwa siku wazazi wanaojifungua 20,huduma kwa wajawazito  wapatao 60 .HV wapatao 25,watoto chini ya miaka 5 wapatao 150 nawengine ni wagonjwa wa magonjwa mbalimbali wakiwepo jinsia zote.

Afisa uhusiano T.B.L  Doris Malulu amesema baada ya kusikia kilio cha wananchi waishiyo Mbagala kuwa wanatatizo kubwa la Maji katika kituo hicho kikiwa kikitoa huduma bora kwa jamii huku akinamama na watoto ndio wameguswa zaidi ndio wenye mahitaji ya maji wakati wa kujifungua.

Malulu amesema T.B.L imejipanga kusaidia shida ya Maji  mikoa yote nchini ambapo imetenga milioni 600 ambazo zitakuwa zikifanya kazi za kusaidia huduma ya maji maeneo ya shule .Vituo vya Afya na vijijini  msaada huu ulianza kutolewa  tangu mwaka huu ulipoanza na kuhitimisha Desembar mwaka huu.

Mganga Mfaudhi Dr Batuli Luhanda wa Mbagala Roundtable Matenity Home Clinic amesema msaada huo umefika wakati muwaka kwa kuwa huduma wameipanua lakini wanakabiliwa na tatizo kubwa la maji baada ya Kisima kilichopo kushindwa kutoa maji ya kutosha baada ya kukauka vyanzo vya maji ,hali hiyo imechangia kurudisha nyuma hutowaji wa huduma kwa wakati.

Dr Luhanda  amewashukuru  Kampuni ya T.B.L kwa kutoa msaada huo utaweza kuwasaidia kwa kutowa huduma iliyo bora kwa kutumia maji safi na salama kwa jamii,pia amehaidi kutunza miundombinu hiyo ya maji ili iweze kutekeleza malengo yaliyokusudia kwa jamii kupata maji salama.

Naye ENG:ONESMO ZAKANA SIGALLA  amehaidi kutengeneza miundombinu ya maji kwa wakati kwa kuwa tatizo la huduma yahapo ikitolewa kwa shida kutokana na hukosefu wa maji katika kituo hicho cha Afya kwa muda mrefu hasa wazazi ndio wamekuwa wakipata shida, amesema hatopenda kuona hali hiyo ikiendelea kwa kuwa ameshakabidhiwa pesa za mradi hivisasa ameanza kazi hatakabidhi kwa wakati,pia hali ya kukauka kwa kisima hicho akitakuwepo.
TBL akikabidhi hundi ya fedha kwa ajili ya uchimbaji wa kisima cha maji kituo cha afya cha Mbagala Roundtable Matenity Home Clinic 

 hundi ya fedha kwa ajili ya uchimbaji wa kisima cha maji kituo cha afya cha Mbagala Roundtable Matenity Home Clinic 

Mganga mfawidhi wa  kituo cha afya cha Mbagala Roundtable Matenity Home Clinic Dr Batuli Luhanda

Mdau wa maendeleo aliyeshiriki makabidhiano ya hundi.



ENG:ONESMO ZAKANA SIGALLA 
Afisa uhusiano T.B.L  Doris Malulu

Kituo cha afya cha Mbagala Roundtable Matenity Home Clinic 

TBL akikabidhi hundi ya fedha kwa ajili ya uchimbaji wa kisima cha maji kituo cha afya cha Mbagala Roundtable Matenity Home Clinic 

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List