MANISPAA YA ILALA NA ZOEZI LA KUWEKA MANISPAA SAFI HUSUSANI SOKO LA KARIA KOO

Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam imewataka wafanya Biashara wadogowadogo maharufu kwa jina la machinga waliokuwepo maeneo sio rasmi  katika soko kuu la kari akoo wafate sheria na taratibu za kufanya biashara kwenye maeneo rasmi lasivyo hatakayebainika akikiuka taratibu zilizowekwa  hatachukuliwa hatua ya faini ya elfu 50 na mali zake kutahifishwa.

Hayo yamesemwa wakati zoezi la upelesheni wa kusafisha mazingira manispaa ya Ilala.zoezi limeanza rasmi ambapo wamejikita katika ukamataji wa machinga wanaofanya biashara maeneo ya Ilala yasiyokuwa rasmi,Usafi wa mazingira kwa nyumba na viwanda vinavyoelekeza maji taka maeneo yasiyo rasmi.pamoja na watu wanaojiusisha na vitendo vya uhalifu.

Mkuu wa Idara ya usafi wa mazingira Manispaa ya Ilala Charles Wambura amewataka Wafanya biashara wote waliopo maeneo ya Ilala wafate sheria zilizopo ili kuepusha lawama kwa Serikali endapo mtu yoyoyte atakaye bahinika akikahidi sheria zilizopo.Pia wananchi wameombwa watoe ushirikiano ili zoezi ilo liweze kufanikiwa.

Mwenyekiti wa zoezi Safisha Manispaa ya Ilala Hassani Mkwawa pamoja na Afisa Mtendaji Kari akoo Sam Swila wamesema zoezi hilo ni endelevu kukumbusha wananchi sheria zilizopo kwa kuwa kwa  muda mrefu wamekuwa wakikahidi na kujiamulia wenyewe,Pia zoezi limelenga kuwakamata watumiaji wa madawa ya kulevya wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu walio maeneo hatarishi.

Wamachinga wakiongea na Mwandishi wa Blog wametupia lawama zoezi hilo la ukamataji ni la unyanyasaji kwa kuwa wapo katika maeneo ya soko  kutokana na kutofanikiwa kumiliki meza kutokana kuwa chache ukilinganisha na Idadi yao.Hata hivyo wameomba watengewe maeneo na sio kutaifishwa mali zao na kupigwa faini.


Pamoja na zoezi hilo la Safisha Manispaa ya Ilala kwa hali ya mazingira bado ni mbaya na mfumo wa maji taka ni wazamani  haukizdhi mahitaji ya hivi sasa kwa wakazi wa manispaa ya Ilala.kutokana hongezeko kubwa la idadi ya Wakazi wa Kariakoo baada ya kujengwa kwa majengo ya ghorofa  wakati miundombinu ya Majitaka bado ni ya zamani na haitoshelezi mahitaji huku ikiwa chakavu.

Bodaboda na biashara zilizokamatwa katika zoezi la weka manispaa safi.

Bodaboda na biashara zilizokamatwa katika zoezi la weka manispaa safi.

Mkuu wa Idara ya usafi wa mazingira Manispaa ya Ilala Charles Wambura


Mwenyekiti wa zoezi Safisha Manispaa ya Ilala Hassani Mkwawa


Lenatusi Ruhungu afisa mtendaji kivukoni.

Bodaboda na biashara zilizokamatwa katika zoezi la weka manispaa safi.

wafanya biashara nje ya soko karia koo wakifanya biashara kwa wasiwasi kutokana na zoezi la ukamataji wa machinga.

Miundombinu mibovu ya maeneo ya karia koo ambapo Manispaa ya Ilala wametaka kuweka safi.

Bodaboda na biashara zilizokamatwa katika zoezi la weka manispaa safi.

wafanya biashara nje ya soko karia koo wakifanya biashara kwa wasiwasi kutokana na zoezi la ukamataji wa machinga.

wafanya biashara nje ya soko karia koo wakifanya biashara kwa wasiwasi kutokana na zoezi la ukamataji wa machinga.
Afisa Mtendaji Karia koo Sam Swila 

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List