Kanisa la Calvary Ass of God Majohe Mikanjuni watoa msaada wa Kitanda cha kinamama Mojohe Dispensary

Jamii nchini       wenye uwezo wa Kipato wameshauriwa kujitolea kusaidia Sekta ya Afya,inakabiliwa na matatizo mengi aswa katika upande wa huduma ya akina mama na Mtoto changamoto kubwa ukosefu wa vifaa vya huduma  vya uzazi kwa akina mama.na sio kuachia kila jambo kufanya serikali pekee.

Hayo yameelezwa katika Kituo cha Afya cha Majohe Dispensary iliyopo wilaya ya Ilala jijini Dar Es salaam baada ya kupokea msaada wa Kitanda cha Kuzalishiwa akinamama wajawazito kimeghalimu milioni moja na laki tano,msaada huo umetolewa  na Kanisa la Calvary Ass of God Majohe Mikanjuni chini ya usimamizi wa Mch,Nabii Amos Peter  Lilai.

Nabii Amos Lilai amesema wameamuwa kutoa msaada kwa wanahoitaji kwa kuwa ndio mpango wa Mungu kusaidia eneo lenye uwitaji ilikutekeleza maandiko Matakatifu,amesema kwakuwa walipata hufahamu kituo hicho kinahukosefu wa Kitanda cha kuzalishia akina mama ndipo walipoguswa na kuona humuimu wa kutoa msaa wa Kitanda cha kuzalishia akinana,lengo kuhepusha vifo visivyotalajia wakati wa kujifungua ili waachane na kulala chini kutokana na hukosefu wa kitanda kimoja.

Dr Elias Mbao wa Majohe Dispensary amesema msaada uliotolewa umefika wakati muwafaka kwa kuwa wanakabiliwa na hupungufu wa Kitanda Kimoja ,kulingana na mahitaji ya hongezeko la huduma za akina mama na mtoto,hatavhivyo walipeleka maombi ya kuongezewa Kitanda kimoja serikalini hivi sasa ni muda mrefu waliambiwa ombi ilo linafanyiwa kazi,ameshukuru kwa Kanisa ilo kutoa msaada huo,hata hivyo ametowa wito kwa watu wengine nao waweze kujitoleya waige mfano wa Kanisa la Calvary Ass of   God Majohe.

Naye mwnyekiti wa akinamama kanisa   hilo la Calvary Ass of God Majohe bi Catherine Massaga ametowa wito kwa Wahuguzi msaada uliotolewa wa Kitanda waangalie na kukitunza  vizuri ili kiweze kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa  kutumia wagonjwa walio wengi huduma ya Kitanda hicho.


Serikali pamoja na jitihada zake kubwa kuboresha sekta ya Afya nchini lakini bado kunachangamoto zinzojitokeza za hupungufu wa Vifaa katika vituo vya Afya nchini,kila mmoja anatakiwa kuguswa na tatizo la Afya na sio kuachia serikali pekee ,hata hivyo msaada huo uliotolewa ulienda sambamba na zoezi la usafi wa Mazingira wa kituo cha afya hicho ,huduma hiyo iliweza kutolewa na Wahumini wa Kanisa la Calva Ass of God Majohe wakishirikiana na Nabii Lilai hilo pia waliweza kuwafariji wagonjwa wote waliokuwepo siku hiyo wakienda sambamba Ibada maarum ya Maombezi.

Kitanda cha kisasa kilichotolewa msaada na Kanisa la Calvary Ass of God Majohe Mikanjuni chini ya usimamizi wa Mch,Nabii Amos Peter  Lilai.
Dr.Elias Mbao wa Majohe Dispensary.

RBECCA J.MBOYA(Nurse incharge)

wakati wa makabidhiano wa kitanda cha kisasa kwa ajili ya kuzalishia wakina Mama watumiaji wa Majohe Dispensary.

Mchungaji na Nabii Amos Peter Lilai.

Dr Elias Mbao wa Majohe Dispensary akihojiwa na waandishi wa Habari.

Catherine Massanga(mwenyekiti wa kinamama CAG majohe)
Jengo la  Majohe Dispensary

wakifanya makabidhiano ya kitanda cha kisasa kwa ajili ya kujifungulia wakinamama.

Wananchi na Waumini walioshiriki siku ya Makabidhiano.

Share on Google Plus

About SDM PRODUCTION MEDIA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List