MBINU MPYA ZATOLEWA ILI KUKUZA MAENDELEO TANZANIA


Mfumo wa fedha wa sasa uliopo nchini unatajwa kuwa miongoni  mwa vikwazo vinavyosababisha wawekezaji wa ndani kushindwa kupata mikopo pamoja na huduma kutoka kwenye taasisi za fedha hivyo wengi kushindwa kuwekeza kutokana na kuwa na  mitaji midogo.

Baadhi ya wawekezaji wenye mitaji ya kati,wameshindwa kuwekeza hasa kwenye miradi mikubwa ya sekta ya nishati,hivyo miradi mingi kuchukuliwa na wawekezaji wan je.

Ni mionguni mwa wawekezaji wanaokutanishwa na mpango huu wa kuwawezesha wawekezaji wa miradi mikubwa na midogo kwenye maeneo ya ufundi na fedha ili kuwasaidia kupata na kuendesha miradi yao wenyewe.

Kwa ushirikiano na Serikali kupitia wizara ya TAMISEMI taasisi ya umoja wa mataifa ya UNCDF ,imekuwa ikiwakutanisha wadau hao wa maendeleo ili kuangalia namna watakavyowawezesha kupata huduma hizo muhimu katika kuboresha miradi yao.

Hata hivyo bado kuna changamoto za kiutendaji kwa wawekezaji hao katika kujihakikishia wanapata misaada hiyo

Mpango huo pamoja na uwezeshaji unalenga kuhakikisha kuwa uwekezaji kwenye miundombinu hususan ya maeneo ya vijijini unaboreshwa ili kusogeza huduma nyingi zaidi kwenye maeneo hayo ambazo kwa sasa zinapatikana zaidi mijini


UNCDF unataraji  kuendelea kutoa huduma zake nchini hadi mwaka 2017 ambapo itaanza kusambaza huduma zake kwenye nchi nyingine Barani Afrka
Wadau wa Maendeleo walioshiriki mkutano wa kupeana maarifa juu ya namna ya kukuza maendeleo.

Wadau wa Maendeleo walioshiriki mkutano wa kupeana maarifa juu ya namna ya kukuza maendeleo.


Wadau wa Maendeleo walioshiriki mkutano wa kupeana maarifa juu ya namna ya kukuza maendeleo.


Wadau wa Maendeleo walioshiriki mkutano wa kupeana maarifa juu ya namna ya kukuza maendeleo.


PETER MALIKA(Chief Technical Advisor)

JUMA .S. SHAMTE(Director of Development)

Wadau wa Maendeleo walioshiriki mkutano wa kupeana maarifa juu ya namna ya kukuza maendeleo.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List