SERIKALI INATAKIWA KUBUNI MBINU YA KUONGEZA MAPATO KUPITIA MISITU NA VIVUTIO VYA ASILI TANZANIA.

Imeelezwa kuwa mchakato wakuiweka Misitu ya safu ya Milima ya Tao la mashariki katika urithi wa Dunia ili kulinda viumbe Hadimu vilivyogundiwa Tanzania hivi karibuni ambavyo viko mbioni kutoweka  huend usifanikiwe kwa kutokana na kuwepo kwa haribifu mkubwa wa Mazingira katika misitu hiyo.

Mchakato huo ambao awali ulikuwa ufanyike na baadae Serikali kuamua kuufuta unaendelea ukiwa na lengo la kulinda na kuhifadhi misitu hiyo.

 Mkurugenzi wa shirika la Hifadhi Misitu ya asili Tanzania Charles Meshack anaiomba Serikali kupititia upya mchakato huo ili uweze kuwa na manufaa kwa Taifa kutokana na kukuza utalii ambao unaliingizia Pato taifa.

Mbali na kuliingizia Taifa Pato la kigeni lakini Misitu hiyo pia inatajwa kuondoa Hewa ukaa inayozalishwa viwandani ambayo uathili viumbe hai vilivyopo nchini.

Aidha katika suala la uhifadhi Misitu pia Serikali nayo ikashauriwa kutoa Elimu kwa wakazi waishio Jirani na Misitu Hiyo ili  kuweza kuepukana na Uharibifu wa mazingira.


Inaelezwa  kuwa Bado kuna Tatizo kubwa la Uelewa kuhusiana na utunzaji wa Mazingira Hali ambayo inatajwa kuhatarisha  kutoweka kwa baadhi ya viumbe hai nchini hali ambayo wataalamu wanasema ipo haja ya kufanya mikakati mbadala ya kunusuru misitu Hiyo.
Displaying ci_84436401_Full.jpg
Moja ya Misitu ya asili yenye kivutio kikubwa nchini Tanzania.
Displaying ci_44388880_Full.jpg
Baadhi ya viumbe wazuri aina ya chura wanaopatikana Tanzania.

Displaying ci_54307400_Full.jpg
Moja ya Misitu ya asili yenye kivutio kikubwa nchini Tanzania.

Displaying ci_63118706_Full.jpg
Baadhi ya viumbe wazuri aina ya kinyonga wanaopatikana Tanzania.

Displaying DSC00336.JPG
Mkurugenzi wa Hifadhi misitu ya Asili Tanzania Ndugu: Charles Meshack

Displaying DSC00338.JPG
Elinasi Monga(Meneja Mradi toka Shirika la kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania)

Displaying DSC00340.JPG
 Gerald kitabu (Mwenyekiti Jukwaa la Waandishi habari Kilimo Tanzania)
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List