Kaimu
Mkurugenzi wa Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika(MISATAN)
Bwana Andrew Marawiti akizungumza jambo wakati akifungua kongamano na
maafisa habari wa taasisi za serikali zilizofanyika jana jijini Dar es
Salaam.
Na Mwandishi wetu
Maafisa
habari mbalimbali kutoka wizara na mihimili tofauti ya nchi, jana
walikutana katika hoteli ya JB Belmont hapa Dar es Salaam kujadili
changamoto wanazo kumbana nazo wakati kwa kutoa taarifa kwa wananchi.
Kongamano hilo linafuatia matokeo ya utafiti wa upatikanaji taarifa kwenye taasisi za umma uliofanywa na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) nakuzinduliwa rasmi siku ya tarehe 28 Septemba, ambayo pia ni Siku ya Kimataifa ya Haki ya Kupata
Taarifa.
Miongoni
mwa taasisi zilizoshiriki katika kongamano hilo ni Bunge, Mahakama,
Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara
ya Nishati na Madini,
Idara ya Habari Maelezo, Mamlaka ya Taifa ya Vitambulisho (NIDA) na Idara ya
Taifa ya Takwimu. Wizara za Afya na Mambo ya Nje hazikuweza kuwakilishwa licha ya kupata mwaliko.
Idara ya Habari Maelezo, Mamlaka ya Taifa ya Vitambulisho (NIDA) na Idara ya
Taifa ya Takwimu. Wizara za Afya na Mambo ya Nje hazikuweza kuwakilishwa licha ya kupata mwaliko.
Mwanasheria
kutoka Taasisi Kitaifa ya Msaada wa Kisheria (National Organization of
Legal Assistance-nola) Bwana James Malenga akisisitiza jambo alipokuwa
anawasilisha mada yake kwenye kongamano hilo la maafisa habari wa
taasisi za kiserikali lililoandaliwa na Misa-Tanzania.
0 comments:
Chapisha Maoni