Rais Kenyatta tayari kwenda ICC

Rais Kenyatta amesisitiza hana hatia na wala hana hofu kuwa mahakama itaamua vinginevyo
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema yuko radhi kwenda katika mahakama ya kimataifa ya ICC kwa kikao maalum kuhusu kesi inayomkabili.
Akiwahutubia wabunge mjini Nairobi,aliwaambia kuwa yuko tayarti kuhudhuria kikao maalum alichotakiwa kuhudhuria mjini Hague bila wasiwasi wowote.
Kenyatta alitakiwa na majaji wa mahakama hiyo kufika ICC tarehe 8 mwezi huu kufafanua madai kuwa serikali yake imekataa kushirikiana na mahakama hiyo hasa upande wa mashitaka kwa kukataa kuipatia ushahidi unaohitajika katika kesi inayomkabili.
Rais Kenyatta anasema anajiamini na kwamba anajua hana hatia katika tuhuma zinazomkabili
Anakabiliwa na tuhuma za kupanga ghasia za kikabila zilizokumba nchi hiyo baada ya uchaguzi wa mwaka 2007/2008.
Aliarifu bunge kuwa anajiamini mwenyewe kiasi cha kuwa tayari kufika mbele ya ICC na kwamba anajua hana hatia katika kesi inayomkabili.
Alisema Kenya ni nchi huru na kwamba haitawahi kuwa chini ya mamlaka nyingine yoyote.
Kenyatta na naibu Rais William Ruto ambaye pia anakabiliwa na kesi katika mahakama ya ICC
Takriban wabunge miamoja wanajiandaa kuambatana na Kenyatta Hague katika ishara yao ya kumuunga mkono.
Uhuru amemkabidhi mamlaka kwa muda naibu wake William Ruto hadi atakaporejea.
Share on Google Plus

About SDM PRODUCTION MEDIA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List