WANANCHI WA TANZANIA KUPEWA MBINU MPYA ZA KUPAMBANA NA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA.

Jamii nchini imeshauriwa kutowanyanyapaa waathirika wa dawa za kulevya nchini kwa kuwa nao ni Wagonjwa kama wagonjwa wengine ingawa huwa na athari za Kisakolojia,kudhoofu Afya ya mwili ,kupoteza mwelekeo wa maisha lakini pia wana Haki sawa kama binadamu wengine.

Wananchi wameombwa kuunga mkono suala la kudhibiti Biashara ya Dawa za kulevya ili kuokoa vijana wanaoteketea kutokana na kutumi Dawa hizo kwani wao ndio nguvu kazi ya Taifa.Akiongezea amesema tatizo la Dawa za kulevya ni la Dunia zima,na Nguvu ya pamoja ndo inaweza kusaidia Mataifa Mbalimbali kupiga Vita Uingizaji wa DAWA ZA KULEVYA pamoja na matumizi yake.Hayo yalizungumzwa na AFISA TAWALA MKUU TUME YA KURATIBU DAWA ZA KULEVYA Bi:AIDA TESHA.

SHIRIKA LA KIMATAIFA LA COMMUNITY ANT.DRUG COALITIONS OF AMERICA(CADCA),limesema uwepo wake Tanzania utasaidia kuongeza nguvu katika kupamabana na Dawa za kulevya kwa kutolewa elimu kwa jamii.CADCA wamesema watatumia njia ya kujenga makubaliano kwa jamii(community coalition)na kumshirikisha kila mtu kwa kuipa nguvu na uamuzi jinsi ya kupambana na Dawa za kulevya.


Tanzania mikoa inayoongoza kwa kuwa na waathirika wa Dawa za kulevya ni pamoja na Dar es salaam,Pwani,Tanga,Mtwara,Morogoro na Arusha.CADCA itashirikiana na SDM PRODUCTION MEDIA kwa kupitia YFSO(Youth friend service) na taasisi ya T-IOGT(Tanzania International organization of good Tamplars) Pomoja na Tume ya kudhibiti Dawa za Kulevya Tanzania.
AFISA TAWALA MKUU TUME YA KURATIBU DAWA ZA KULEVYA Bi:AIDA TESHA.


ERIC SIERVO,M.ED.(Senior Manager CADCA)

COLBER PROSPER(SENIOR CONSULTANT PROSPER &PARTNERS)

CADCA TEAM baada ya Kikao.

Wadau wa kupambana dhidi ya Dawa za kulevya wakipeana Mkono baada ya kikao.

Picha ya Pamoja baada ya kumaliza kikao.

Picha ya Pamoja baada ya kumaliza kikao.



Share on Google Plus

About SDM PRODUCTION MEDIA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List