CCM WAJIPANGA KUSHINDA KWA KUSIMAMISHA VIONGONZI WANAOKUBALIKA NA WANANCHI NA CHAMA



Makamamu wa Rais Dkt Ghalib Bilali amewataka viongozi wa chama cha mapinduzi-CCM ngazi ya wilaya na mkoa kuhakikisha wanakuwa makini katika uteuzi wa kuraa za maoni na kuhakikisha mgombea anayeteuliwa anakubalika ndani ya jamii.

Dkt Balali ametoa tahadhali hiyo ikiwa ni siku 30 tu zimesalia kuanza kwa harakati za uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika Desemba 14 mwaka huu.

Amesema katika Uchaguzi wa mwaka 2009/10 katika Mchakato wa Kura za Maoni zilijitokeza Kasoro zilizotokana na uchaguzi wa Wagombea wasiokubalika na Jamii, Hali iliyopelekea CCM kupoteza nafasi zake nyingi na hivyo kuchukuliwa na upinzani

Dkt Bilali amesema nia ya Chama cha mapinduzi ni kuhakikisha wanapata ushindi wa kishindo hivyo akawataka Viongozi wa CCM kuhakikisha wanaepuka Malalamiko katika uteuzi wa kura za maoni na kuyafanyia kazi
Akifungua mkutano Halmashauri ya CCM Mkoa wa Dar es salaam, uliyojadili namna ya kushiriki kwenye chaguzi za serikali za mitaa, Dkt Bilali ambaye pia ni mlezi wa Mkoa huo kichama amesema silaha kubwa ya ushindi ni kuchagua mgombea anayekubali.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam, CCM Ramadhan Madabida akatoa msimamo wa chama hicho katika kuhakikisha kasoro hizo hakizijitokezi.

Hadi sasa tayari wagombea 2519 wamejitokeza kugombe nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi za serikali za mitaa  na kwa mujibu wa CCM Mkoa wa Dar es salaam, Novemba 16 hadi 17 ndiyo siku ya kuanza uteuzi wa kura za maoni kwa wagombea kupitia chama hicho.










Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List