WASICHANA WANATAKIWA WAWASIKATE TAMAA NA MAISHA, WAJITUME WATAFANIKIWA


Wasichana waishio katika mazingira hatarishi wamepatiwa mafunzo mbalimbali ya ujasiriamali ikiwemo ufundi ushonaji ili kuwasaida waweze kujipatia kipato
na kuachana na tabia hatarishi ya kujipatia kipato kwa kufanya ngonozembe .

Mafunzo hayo yametolewa bure na  Asasi ya Chagua Maisha iliyopo Jijini Dar Es Salaam kwa wasichana zaidi 165 wanaoishi kwenye mazingira hatarishi kutoka Yombo,Mbagala na Chanika Jijini Dar Es Salaam kwa lengo la kubadili maisha yao  Kiuchumi  na kimaadili ili wawe mfano kwa jamii


Miongoni mwa kumbukumbu mbaya ambazo zitaendelea kubaki vichwani mwa wanawake wengi waliotumbukia katika biashara ya uuzaji miili yao

Eneo la uwanja wa fisi lililopo katikati ya jiji la Dar es Salaam maarufu kwa biashara ya ukahaba. Hili ni miongoni mwa madangulo mengi yaliyotapakaa sehemu mbalimbali nchini ambapo kila aina ya uhalifu unafanyika hapa tena hadharani na kwa wakazi wa eneo hili kwao ni matukio ya kawaida kabisa.

Huenda changamoto za ugumu wa maisha ndizo zinazopelekea vijana wengi haswa wasichana kukata tamaa na kuamua kujiingiza kwenye biashara ya uuzaji miili yao wakiamini huenda wakapata ahueni ya kimaisha na kujikwamua kiuchumi ili waweze kujikimu walau kwa mahitaji yao madogomadogo ya kila siku ndoto ambayo inabaki kuwa kiza kinene kwa walio wengi kwani badala yake huambulia magonjwa mbalimbali ya ngono ikiwemo maambukizi ya virusi vya Ukimwi

Na sasa wapo wanaojutia ingawa kwao matumaini yamerejea baada ya kusaidiwa kutoka katika sehemu hizo hatarishi na wameamua kuanza maisha mapya huku wakiwataka wenzao pia wajitokeze hadharani ili wapatiwe msaada.


Bi Johari Sadick yeye ni mlezi wa wanawake hawa.

Wasichana wa kike zaidi ya 165  waliojitokeza hadharani wanapatiwa msaada wa mafunzo ya kiujasiliamali katika kituo hiki kipya cha ufundi kushona na wanapatiwa pia elimu ya vvu na ukimwi ili wasiweze tena kurudi katika biashara hiyo huku wito ukitolewa kwa vijana wengi zaidi kujiepusha na makundi hatarishi


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List