MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA TRA IMETOA TUZO KWA WALIPA KODI WAZURI


Waziri Kiongozi  mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Shamshi Vuai Nahondha amesema Serikali inakusudia kuanzisha Sheria mpya ya kodi itakayokuwa na msukumo rafiki kwa wafanyabiashara kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa hiari na wakati.

Akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya mlipa kodi Jijini Dar Es salaam, Nahodha, amesema uanzishwaji wa sheria hiyo ni mpango Mkakati wa Serikali kutaka Nchi iwe na mfumo mmoja wa ukusanyaji kodi.

Amesema sheria iliyopo sasa ya ukusanyaji kodi imetoa mwanya mpana wa kuruhusu kuwa na kodi nyingi ambazo zimesababisha walipa kodi wengi kutokuwa rafiki wa ulipaaji kodi kama ilivyo kwa nchi zilizoendelea.

Kwa kutambua hilo hivi sasa nchi imeweka misingi imara ya ukusanyaji kodi kwa kuwa na mfumo mmoja utakahusisha maeneo yote ya ukusanyaji ikiwemo serikali kuu na halmshauri.

Kwa upande wake Naibu waziri wa Fedha Adam Malima amesem nia ya serikali ni kuona Nchi inakuwa na uchumi mzuri unaotokana na ulipaji kodi za ndani lakini mafanikio yake bado yanachangamoto

Novemba 21 kila mwaka ni siku ya mlipa kodi, Mamlaka ya mapato nchini ndiyo wenye dhamana na siku hiyo, Rished Bade ni Kamshina Mkuu wa TRA,mpango wa mamlaka yake kuanza kutumia mfumo wa Teknohama kama njia mkakati ya kuwa na makusanyo mazuri.


































Maadhimisho hayo ni ya nane kufanyika na kwa kupitia siku ya mlipa kodi Serikali imeweka lengo kuhakikisha inakusanya Mapato yatokanayo na Kodi yanafikia shs Trioni 11.9 kwa mwaka wa fedha 2014/15  mwisho 


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List