SOMA ALICHOKISEMA PROF. MUHONGO ALIPOTANGAZA KUJIUZULU


Na Chalila Kibuda, Dar
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhuongo, amejiuzulu wadhifa huo kutokana na kuchoshwa na sakata la Akauti ya Tegeta Escrow.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, Barabara ya Samora, Profesa Sospeter Muhongo amesema ameamua kujiuzulu ili kuwa sehemu ya suluhisho la suala la akaunti ya Tegeta Escrow.

Aidha Muhongo alisema kuwa suala la ankauti ya Tegeta Escrow limekuwa likizungumzwa na kufanya mambo mengine yasiendelee na huku watanzania walio wengi ni masikini wakihitaji umeme na sio kuuliza tegeta Escrow.

"Suala hili mimi nililikuta toka mwaka 2012 na sijaweza kuchukua fedha katika ankauti ya Tegeta Escrow, mimi sio mla rushwa, mimi sio mwizi na hakuna mtu yeyote anayeweza kunipatia rushwa, 

“Akaunti ya Tegeta Escrow ilitawaliwa na mvutano wa kisiasa, kibiashara, ubinafsi, uongozi na madaraka sasa watu wakae kujadili masuala mengine hata bunge litumie muda kujadili mambo  mengine  pamoja na Chama cha Mapinduzi (CCM) kinatumia muda mwingi kujadili suala la Escrow.

Hivyo nimeamua kujiuzulu nafasi ya uwaziri ili niweze kuwa sehemu ya bunge na kuendelea kuchangia katika masuala ya maendeleo kwani suala la escrow sio suluhisho kwa watanzania". Alisema Muhongo

Muhongo alisema kuwa anashukuru sana kwa kushirikiana vizuri na makamu wa Rais, Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na baraza la mawaziri.

Aidha alisema kuwa kuchelewa kujiuzulu alitaka wananchi wajiridhishe pamoja na kumalizia kazi zingine ambazo zilikuwa mezani kwake ili zikamilike hivyo asingeweza kufanya halaka kwani anajiamini kuwa ni mchapakazi na muadilifu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Inaendeshwa na Blogger.

Wanaofuata

TANGAZO

My Blog List